Sports
Aldrine Kibet Kujiunga Rasmi Na Celta Vigo Ya Uhispania

Kiungo wa Harambee Stars chipukizi marufu kama Junior Stars Aldrine Kibet sasa ni rasmi anajiunga na kilabu ya Celta Vigo inayoshiriki ligi ya Laliga msimu ujao baada ya wazazi wake kusafiri kuelekea uhispania kukamilisha dili hiyo ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19.
Kibet ambaye alitoka shule ya Upili ya St.Anthony ya Kitale alijiunga rasmi na Akademia ya Nasty mwaka jana ambapo amepata ufanisi mkubwa mno pamoja na beki Amos Wanjala.
Mchezaji huyo mbunifu amewakilisha Junior Stars katika mashindano ya CECAFA na kombe la Bara Afrika mjini Cairo Misri mwezi Mei mwaka huu.
Mchanaji huyo awali na sasa bado ana imani ya kuchezea kilabu ya Barcelona na kuwa mkenya wa kwanza kuchezea mwabingwa hao wa Uhispania.
Sports
Makocha Saba pekee Wameshinda Taji La CHAN

CHAN COUNT DOWN 16 Days to Go
Sports
Matumaini Ya United Kupata Mbeumo Yanazidi Kudidimia

Matumaini ya kilabu ya manchester united kupata huduma za kiungo mshambulizi wa kilabu ya Brenford Bryan Mbeumo yanaonekana kufifia kila kuchao.
Haya yanajiri baada ya mazungumzo hayo kukwama kwa sasa baada ya kilabu hiyo ya London kuongeza ada ya malipo ya mchezaji huyo hadi pauni milioni 70.
Kilabu ya Manchester United haiko tayari kulipa zaidi ya pauni milioni 65 kwa mvamizi huyo raia wa Cameroon.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alifunga magoli 20 ligi ya epl msimu jana.