Sports
Aldrine Kibet Kujiunga Rasmi Na Celta Vigo Ya Uhispania

Kiungo wa Harambee Stars chipukizi marufu kama Junior Stars Aldrine Kibet sasa ni rasmi anajiunga na kilabu ya Celta Vigo inayoshiriki ligi ya Laliga msimu ujao baada ya wazazi wake kusafiri kuelekea uhispania kukamilisha dili hiyo ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19.
Kibet ambaye alitoka shule ya Upili ya St.Anthony ya Kitale alijiunga rasmi na Akademia ya Nasty mwaka jana ambapo amepata ufanisi mkubwa mno pamoja na beki Amos Wanjala.
Mchezaji huyo mbunifu amewakilisha Junior Stars katika mashindano ya CECAFA na kombe la Bara Afrika mjini Cairo Misri mwezi Mei mwaka huu.
Mchanaji huyo awali na sasa bado ana imani ya kuchezea kilabu ya Barcelona na kuwa mkenya wa kwanza kuchezea mwabingwa hao wa Uhispania.
Sports
Mabondia Kutoka Vilabu Mbalimbali Nchini, Kuzindua Uhasama Mjini Mombasa

Zaidi ya mabondia 180 wa kiwango cha juu kutoka vilabu 26 kote nchini wanatarajiwa kushiriki mashindano ya ndondi ya mzunguko wa pili Kenya yanayotarajiwa kuanza hii leo hadi 19 mwaka huu yatakayoandaliwa katika taasisi ya Alliance Francaise jijini Mombasa.
Miongoni mwa mabondia watakaoshiri mashindano hayo ni Bonface Mogunde wa huduma ya polisi nchini ambaye hajapoteza pambano katika uzani wake, mshindi wa dhahabu kwenye Michezo ya Afrika Edwin Okongo wa KDF mabondia wa Mombasa, Kombo Mwinyifaki na Shaffi Bakari, pia watapanda ulingoni.
Mashindano hayo yameandaliwa na chama cha Ndondi cha Kaunti ya Mombasa kwa ushirikiano na taasisi ya Alliance Française kama sehemu ya mradi wa ushirikiano wa michezo kati ya Kenya na Ufaransa uitwao Ndondi Mashinani, kwa usaidizi wa Ubalozi wa Ufaransa.
Michuano hiyo inalenga kukuza vipaji, hasa kwa wanawake na vijana, pamoja na kuandaa wawakilishi wa Mombasa kwa mashindano ya Olimpiki yajayo.
Sports
Kiungo Wa Junior Stars Aldrine Kibet Ni Mali Ya Celta Vigo
