Sports
Alcaraz,Sabalenka ndaani ya Robo Fainali,Wimbledon

Bingwa mtetezi wa Wimbledon na mchezaji anayeorodhshwa wa pili ulimwneguni kwa sasa mchezo wa Tennis Carlos Alcaraz raia wa Uhispania pamoja na Aryna Sabalenka anayeotodhshwa wa kwanza upande wa akina dada wamejitosa katika robo fainali mashindano ya Wimbledon Uingereza.
Alcaraz sasa atamenyana na Cameron Norris raia wa Uingereza akitarajiwa kuingia kwenye daftari za kumbukumbu kwa kuwa miongoni mwa wachezaji ambao wameshinda msururu huo kwa miaka mitatu mfululizo wengine ambao wamewahi kushinda mara tatu kwa mpigo ni pamoja na;Bjorn Borg, Pete Sampras, Roger Federer and Novak Djokovic.
Kwa upande wake nyota wa upande wa akina Aryna Sabalenka baada ya kushinda mechi zake zote sasa ameratibiwa kumenyana na Laura Siegemund akisaka taji la nne la Grand Slam kule Wimbledon.
Sports
Harambee Stars Kundi La Kifo Kundi B.

Sports
Kiungo Wa Brenford Bryan Mbeumo Sasa Ni Mali Ya United

Baada ya vute ni kuvute ambayo imedumu kwa kipindi cha mwezi mmoja ni rasmi kwamba kilabu ya manchester United na Brenford wameafikia makubaliano ya pauni milioni 70 ya kiungo mshambulizi Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.
Haya yanajiri baada ya ofa mara mbili ya united kukataliwa na kilabu hio kabila ya kutuma ofa ya mwisho ya pauni milioni 65 na nyongesa ya pauni milioni 5.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano baada kukubali matakwa yake binafsi.
Mbeumo anakua sajili wa pili kwa kocha mkuu Ruben Amorim baada ya ujio wa mshmabulizi Matheus Cunha.