Connect with us

News

Achani, Aagiza wizara 10 zilizogatuliwa kupeana kandarasi kwa Vijana

Published

on

Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani ameagiza wizara 10 zilizogatuliwa katika serikali za kaunti kupeana kandarasi za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa makundi ya akinamama na vijana katika kaunti hiyo ili kukabiliana na suala la ukosefu wa ajira na kupunguza viwango vya umaskini.

Kulingana na Gavana Achani, kufikia sasa jumla ya kampuni 300 za akina mama na vijana zimesajiliwa huku kampuni 105 zikipewa kandarasi za ujenzi wa zahanati, shule za Chekechea, upanuzi wa mabomba ya maji miongoni mwa kandarasi zengine.

Gavana Achani alisema hatua hiyo itasaidia wakaazi wa Kwale kujiajiri na kupunguza viwango vya umaskini.

“Nilisema akina mama na vijana waunde kampeni ili tuweze kujiajiri kwani hali ya uchumi kwa sasa hivi ni mbaya kwani saa hizi pale serikali ya kaunti imefikishwa haiwezi kuajiri na ni lazima tutafute njia mbadala za ni vipi watu watawezepata nafasi za ajira”, alisema Achani.

Gavana Achani awakabidhi vijana cheti cha usajili wa kampuni.

Kwa upande wake Katibu wa Wizara ya Huduma za Jamii na Ukuzaji Talanta katika serikali ya kaunti ya Kwale Riziki Mwasoza alisema kuwa wamekuwa wakiwapa mafunzo kina mama na vijana waliosajili kampuni na kuwajimiza kutumia kampuni hizo kusaka zabuni katika mashirika ya kibinafsi.

“Kama idara mwaka uliopita tuliwafanyia mafunzo akinamama na vijana ya siku tatu ili kujua jinsi ya kusimamia mapato yao”, alisema Mwasoza.

Nao wakaazi ambao wanamiliki kampuni na waliofaidika na kandarasi za serikali ya Kwale wakiongozwa na Mathew Kailu kutoka Shimbahills alieleza kwamba tangu wasajili kampuni hizo wamepata zabuni za hadi shilingi milioni 9 zinazowapa faida kubwa na kufanya miradi mbali mbali ya kuwajimu kimaisha.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Serikali yaombwa kuondoa miili 400 hospitali ya Malindi

Published

on

By

Kamati ya afya ya bunge la seneti sasa imetoa wito kwa serikali kuu kuiondoa miili zaidi ya 400 ambayo inaendelea kuhifadhiwa katika makafani ya hospitali ya Malindi kaunti ya Kilifi baada ya kufukuliwa katika msitu wa Shakahola.

Akizungumza kwa niaba ya kamati hiyo, seneta wa kaunti ya Bungoma David Wakoli, alisema maiti hizo zimezuia serikali ya kaunti ya Kilifi kuendeleza ujenzi wa makafani mpya katika hospitali hiyo.

Wakoli alisema ikiwa serikali itazingatia hilo basi serikali ya kaunti ya Kilifi itaweza kujenga makafani hiyo bila changamotoz zozote.

“Tunataka kuiomba serikali kuu kuruhusu serikali ya kaunti ya Kilifi kuendeleza ujenzi huo, na serikali inapaswa kutafuta eneo maalumu la kuhifadhi na kuizika miili hiyo’’ Alisema Wakoli

Hii ni baada ya serikali kutenga fedha katika bajeti ya mwaka jana ili kujenga makafani mpya kushindwa kuendeleza ujenzi huo kutokana na miili ambayo bado haijatambuliwa.

Ni kauli ambayo iliungwa mkono na seneta wa kaunti ya Kilifi Stewart Madzayo ambaye aliitaka serikali kuu kukamilisha shughuli ya uambatanishaji wa chembechembe za msimbojeni-DNA, ili kupeana miili hiyo kwa wapendwa wao kabla ya kuanza kufukua miili mingine katika eneo la Kwa Binzaro huko Shakaholo.

“Kule Shakahola tumeona watu wanaendelea kufa na wengine kuzikwa, kwahivyo tunaomba zile maita ambazo ziko hapa ziweze kuondolewa na serikali kuu maana hakuna nafasi,’’ alisisitiza Madzayo.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Rais Ruto amteua Amani Yuda Komora kuwa Mwenyekiti wa NPSC

Published

on

By

Rais William Ruto amemteua Amani Yuda Komora kuwa Mwenyekiti wa Tume ya kitaifa ya Huduma ya Polisi (NPSC) na Angeline Yiamiton Siparo kuwa mwanachama.

Uteuzi huo unafuatia mahojiano ya hivi majuzi yaliyofanywa na Tume ya Utumishi wa Umma (PSC) kati ya Julai 1 na Julai 3 2025, baada ya kuorodhesha wagombea wanane wa uwenyekiti na 11 wa wajumbe.

Wawaniaji walitakiwa kuwasilisha kitambulisho halisi cha kitaifa, hati za masomo, na idhini halali kutoka kwa mashirika ya serikali.

Stakabadhi nyingine ilikuwa ni pamoja na nyaraka za mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini (KRA), tume ya maadili na kupambana na ufisadi (EACC), fomu maalum kutoka kwa mkurugenzi wa idara ya upelelezi wa jinai (DCI), bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HELB) na ofisi yoyote iliyosajiliwa ya marejeleo ya mikopo.

Wale walio na shahadi ya digrii za mataifa ya kigeni walilazimika kuwasilisha barua za utambulisho kutoka kwa tume ya elimu ya vyuo vikuu.

Shughuli ya uteuzi ilianza mnamo mwezi Februari baada ya kujiondoa kwa tume ya awali, inayoongozwa na Eliud Kinuthia, ambaye muhula wake wa miaka sita ulimalizika mapema mwaka huu wa 2025.

Iwapo itaidhinishwa na Bunge, NPSC itajumuisha Komora kama Mwenyekiti na wanachama watano wakiwemo, Peris Muthoni Kimani, Edwin Cheluget, Benjamin Juma Imai, Collete Suda na Angeline Yiamiton Siparo

Komora ni naibu mwenyekiti wa zamani wa tume ya kutathmini mishahara na marupurupu ya wafanyakazi wa umma (SRC), na hapo awali alikuwa na majukumu ya juu ya rasilimali watu katika Mamlaka ya Bandari KPA na KRA.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending