Connect with us

News

Viongozi wa Kilifi Wapinga Uekezaji wa Mradi wa Kawi ya Nuklia

Published

on

Wizara ya Kawi nchini imefanya kikao cha mazungumzo na uongozi wa kaunti ya Kilifi, pamoja na wabunge na Wasimamizi wa Shirika la NUPEA kuhusu uekezaji wa mradi wa uzalishaji kawi ya Nuklia katika kijiji cha Uyombo wadi ya Matsangoni katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini katika kaunti ya Kilifi.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kikao hicho mjini Kilifi, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi amesema japo viongozi wa kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi hawajaridhishwa na uekezaji wa mradi huo, mazungumzo kuhusu mradi huo bado yataendelea ili kuibuka na mwafaka kwani utasaidia pakubwa katika uzalishaji kawi.

Kwa upande wake Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro amesema msimamo wa serikali ya kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi bado uko pale pale wa kuendelea kupinga uekezaji wa mradi huo wa mabilioni ya pesa, akisema utafiti uliofanywa umebaini kwamba mradi huo unaathari kubwa kwa wananchi.

Hata hivyo Mbunge wa Kilifi Kazkazini Owen Baya amesema kama viongozi kutoka kaunti ya Kilifi hawako tayari kupokea mradi huo wa uzalishaji kawi ya Nuklia, akisema changamoto nyingi bado hazitatuliwa katika mradi huo ambazo ni athari kwa wananchi.

Kikao hicho hata hivyo kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Malindi Amina Mnyazi, Mbunge wa Kaloleni Paul Katana, Mbunge wa Kilifi Kusini Ken Chonga, Mbunge wa Ganze Kenneth Tungule, Katibu katika Wizara ya masuala ya vijana na michezo nchini Fikirini Jacobs miongoni mwa viongozi wengine.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Gor Mahia Yailaumu Fkf Kutokana Na Vurugu Gusii

Published

on

By

Mabingwa mara 21 ligi kuu humu nchini kilabu ya Gor Mahia imeilaumu shirikisho la soka nchini FKF pamoja na kamati inayosimamia ratiba ya mechi za ligi kuu kutokana na vurugu iliyoshuhudiwa ugani Gusii wikendi.

Kupitia barua kilabu hiyo imelaani kitendo hicho huku ikisema kwamba shirikisho pamoja na wasimamizi wa ligi hiyo waliwapuuza kutokana na ubora wa uwanja huo kuandaa mechi kubwaa kama hiyo ila wakapuuza kabisaa.

Kulingana na katibu mkuu wa kilabu ya Gor mahia Nicanor Arun ni kwamba hawatachezea tena uwanjani humo siku zijazo wakilaumu mashabiki wa Shabana kwamba ndio walianza vurugu hiyo ugani Gusii.

Katibu huyo aliendelea kusema alishangaa licha ya kamanda wa mechi hiyo kutaka mechi hiyo kuhairisha viongozi wa Shabana walisisitiza mechi iendelee kama ilivyopangwa.

Takwimu ambazo zimetolewa na maafisa wa usalama ni kwamba zaidi ya watu 72 waliweza kutibiwa baada ya kujeruhiwa kwenye vurumahi hio kogalo wakiponyoka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya wapinzani wao Shabana.

Continue Reading

News

Trent Arnold Aondoka Anfield

Published

on

By

Beki wa taifa la Uingereza Alexander Trent Arnold ametangaza kugura kilabu ya Liverpool baada ya msimu huu kukamilika. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ametangaza kugura kilabu hiyo baada ya kuhudumia kwa zaidi ya miaka 20 akitokea kwenye akademia ya The Reds.

kwenye kanda aliyopost kwenye mitandao yake ya kijamii beki huyo wa kulia ameshukuru kilabu hio na mashabiki wake kwa nafasi na ungwaji mkono ambao walimpa tangu akiwa  mchezaji mdogo kilabuni humo.

TAA amefanikiwa kufunga magoli 18 na kuwa beki aliyechangia kupiga basi nyingi epl akiwa amepakua pasi 64 kwa wenzake kufunga,akiwa ameshinda mataji 2 ya Epl moja ya kilabu bingwa ulaya miongoni mwa mataji mengine.

Inaaminika mchezaji huyo tayari amekubaliana na uhamisho wa bila malipo na kilabu ya Real Madrid baada ya kudinda kutia wino mkataba mpya na The Reds akiwa tayari amekubaliana na matakwa yake binafsi.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.