Connect with us

News

Viongozi wa Kilifi Wapinga Uekezaji wa Mradi wa Kawi ya Nuklia

Published

on

Wizara ya Kawi nchini imefanya kikao cha mazungumzo na uongozi wa kaunti ya Kilifi, pamoja na wabunge na Wasimamizi wa Shirika la NUPEA kuhusu uekezaji wa mradi wa uzalishaji kawi ya Nuklia katika kijiji cha Uyombo wadi ya Matsangoni katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini katika kaunti ya Kilifi.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kikao hicho mjini Kilifi, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi amesema japo viongozi wa kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi hawajaridhishwa na uekezaji wa mradi huo, mazungumzo kuhusu mradi huo bado yataendelea ili kuibuka na mwafaka kwani utasaidia pakubwa katika uzalishaji kawi.

Kwa upande wake Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro amesema msimamo wa serikali ya kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi bado uko pale pale wa kuendelea kupinga uekezaji wa mradi huo wa mabilioni ya pesa, akisema utafiti uliofanywa umebaini kwamba mradi huo unaathari kubwa kwa wananchi.

Hata hivyo Mbunge wa Kilifi Kazkazini Owen Baya amesema kama viongozi kutoka kaunti ya Kilifi hawako tayari kupokea mradi huo wa uzalishaji kawi ya Nuklia, akisema changamoto nyingi bado hazitatuliwa katika mradi huo ambazo ni athari kwa wananchi.

Kikao hicho hata hivyo kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Malindi Amina Mnyazi, Mbunge wa Kaloleni Paul Katana, Mbunge wa Kilifi Kusini Ken Chonga, Mbunge wa Ganze Kenneth Tungule, Katibu katika Wizara ya masuala ya vijana na michezo nchini Fikirini Jacobs miongoni mwa viongozi wengine.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Jefwa, Afikishwa Mahakamani kwa Kumjeruhi Mwanamke

Published

on

By

Mwanamume mmoja amefikishwa katika Mahakama ya Kilifi kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi mwanamke kwa kisingizio cha uchawi.

Mahakama imearifiwa kwamba mnamo tarehe 6 mwezi Disemba mwaka 2024, mshukiwa kwa jina Jefwa Kambengu Leso, alimvamia mlalamishi Dama Mkare Lewa akiwa njiani na kumpiga hadi kumjeruhi.

Mahakama imeelezwa kwamba mshukiwa alimziba pua na mdomo mlalamishi ili kuzuia asipige kelele na kufanikiwa kutekeleza kitendo hicho katika eneo la Mdzongoloni Wadi ya Tezo katika kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa, ameagiza mshukiwa wa kesi hiyo kufika Mahakamani mnamo tarehe 14 mwezi Julai mwaka huu pamoja na kuagizwa kusitisha vitisho dhidi ya mlalamishi.

Continue Reading

News

Oburu, Awakosoa Wanaopinga Ushirikiano wa Rais Ruto na Raila

Published

on

By

Seneta wa kaunti ya Siaya, Oburu Oginga amejitokeza na kutetea ushirikiano wa utendakazi kati ya Rais William Ruto na Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga, akisema umeunganisha sehemu ya upinzani na serikali.

Oburu amebainishwa kwamba ushirikiano huo utasaidia kufanikisha utoaji wa huduma bora kwa wakenya wote na haufai kukosolewa.

Oburu amesema viongozi ambao wanaandaa uvumi dhidi ya mpango huo wa ushirikiano wa utendakazi wana malengo mabaya ya kusambaratisha maendeleo, akiwataka kuruhusu eneo la Nyanza kunufaika kimaendeleo.

Kwa upande wake Kiongozi wa walio wachache katika bunge la kitaifa na ambaye pia ni mbunge wa Suna Mashariki Junet Mohammed amewasuta wale wanaopinga ushirikiano huo, akiwataka kupeyana nafasi kwa wakenya kunufaika kimaendeleo.

Hata hivyo Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi ameweka wazi kwamba eneo la Nyanza litaendelea kuunga mkono serikali ya Kenya kwanza kwa manufaa ya wananchi wote.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.