Connect with us

Sports

Mancity Inamnyemelea Kiungo Tijjani Reijnders

Published

on

Kilabu ya Manchseter City iko kwenye mazungumzo ya moja kwa moja na kiungo wa AC Milani Tijjani Reijnders kumleta ugani Etihad msimu ujao.

Mawakala wa mchezaji huyo wanataka kitita cha pauni milioni 60 kumwachilia mholanzi huyo ambaye amefunga magoli 19 katika mechi 104 ambazo amechezea Milan

Hata hivyo city wako tayari kutoa pauni milioni 55 kupata sahihi yake  na kumpa kandarasi nono mkataba wa miaka mitano ugani Etihad.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alijiunga na Milan msimu jana akitokea AZ Alkamar ya Eredivise.

City wangali sokoni kupata mrithi wa kiungo mbunifu Kevin De Bruyne ambaye ameondoka kwenye kilabu hiyo baada ya mafanikio makubwa ikidaiwa pia wanamfukuzia kiungo wa Lyon Ryan Cherki raia wa Ufaransa.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Bruno Akataa Al-Hilal

Published

on

By

Ni taarifa nzuri kwa mashabiki wa kilabu ya Manchester United kwani ,Kiungo na nahodha wa kilabu ya Manchester united Bruno Fernandes amekataa ofa ya pauni milioni 200 kutoka kilabu ya Al-Hilal ya saudia.

Mabingwa hao walikua wametoa ofa hiyo na ada ya ununuzi ya pauni milioni 100 kwa kilabu ya United kupata sahihi ya mchezaji huyo ila inaaminika familia imekua sababu kuu ya Mreno huyo kudinda kuondoka england.

Timu hiyo ilikua imempa kiungo huyo makataa ya wiki moja kuamua iwapo atajiunga nao au la. Hata hivyo baada ya kuketi mezani na mawakala wake na kilabu ya Manchester United inaaminika kwamba mchezaji amekubali kusalia barani Ulaya.

Kilabu ya Al-Hilal ilikua tayari kumpa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 mkataba wa miaka mitatu na mshahara mnono kujiunga nao msimu ujao ila uwamuzi huo umepokelewa vyema na usimamizi wa United ambao hawakua tayari kumwachilia nyota huyo.

 

Continue Reading

Sports

Ligi Limetuponyoka Asema Zico

Published

on

By

Mkufunzi wa Kilabu ya Gor Mahia Zedekiah Zico Otieno amekubali kwamba ligi imewaponyoka baada ya kutoka sare na kilabu ya Afc Leopards ugani raila odinga katika debi la Mashemeji jana jioni.

Kiungo matata Austine Odhiambo aliweka uongozini Kogalo kipindi cha kwanza dakika ya 30 kabila ya Brian wanyama kuisawazishia chui dakika ya 55 kipindi cha pili na kocha huyo anaamini taji limewatoka baada ya sare hiyo inayowacha nafasi ya tatu.

“Tulianza Vizuri lakini concetration lapse imetucost kipindi cha pili,lengo letu lilikua kupata ushindi hapa ili kuweka pressure kwa viongozi lakini sasa matokeo haya ni ishara tosha sasa itabidi tuangazie taji la Mozzartbet Cup.”

Kwa upande wake Mkufunzi wa Afc Leopards Fred Ambani amesema kwamba ameridhishwa na matokeo hayo akijigamba angali kupoteza mechi ya Debi akiwa mchezaji na sasa kama kocha wa Ingwe.

“Vijana walioanza mechi kwa mchecheto na uoga mwingi katika kipindi cha kwanza ila tulipoenda katia dressing room nikawambia watulie na ndiposa tukarejea mchezoni,ningali kupoteza debi kama mchezaji sikuwahi na sasa kama kocha pia bado sijapoteza.

Gor inasalia ya tatu na alama 55 huku Afc Leopards wakibaki ya sita na alama 47.

 

Continue Reading

Trending