Connect with us

Business

Wafanyabiashara wa Matunda Malindi Walalamikia Kudorora kwa Biashara Kutokana na Ukosefu wa Soko

Published

on

Wafanyabiashara wa kuuza matunda karibu na soko la Kwa Jiwa mjini Malindi, Kaunti ya Kilifi, wanalalamikia kushuka kwa biashara yao kutokana na uhaba wa wateja katika eneo hilo.

Akizungumza na mwanahabari wetu, Mshauri Mkuu wa chama cha Matunda Sales Group, Nathaniel Menza Chengo, amesema kuwa matunda yao yanaendelea kuharibika kila siku kwa kukosa wanunuzi, hali ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kudorora kwa biashara zao.

“Kwa sasa matunda ni mengi lakini hakuna soko. Tunapata hasara kubwa kwa sababu matunda yanaharibika kabla hatujayauza,” amesema Chengo.

Chengo ameitaka serikali ya kitaifa pamoja na serikali ya Kaunti ya Kilifi kuchukua hatua za haraka kwa kujenga kiwanda cha kusindika matunda ili kuwawezesha kuuza bidhaa zao kupitia viwandani. Anasema hatua hiyo itasaidia kupunguza hasara na kuinua maisha ya wafanyabiashara katika eneo hilo.

Amebainisha kuwa kwa sasa, zaidi ya tani 10 za matunda huharibika kila siku kutokana na ukosefu wa soko la uhakika.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wadau wa Sekta ya Uchumi wa Baharini Waisihi Serikali Kuongeza Uwekezaji Pwani

Published

on

Wadau katika sekta ya uchumi wa raslimali za baharini na maziwa katika eneo la Pwani wameitaka serikali kuongeza uwekezaji katika sekta hiyo ili kusaidia kuongeza nafasi za ajira kwa vijana wa eneo hilo.

Kwa mujibu wa wadau hao, serikali haijatoa kipaumbele cha kutosha kwa sekta hiyo, licha ya kuwepo kwa raslimali nyingi za bahari ambazo bado hazijatumika ipasavyo. Wamesisitiza kuwa uwekezaji wa kimkakati unaweza kufungua fursa nyingi kwa vijana, na hivyo kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira katika ukanda wa Pwani.

Viongozi hao pia wameitaka serikali, kupitia wizara husika, kuweka mikakati ya wazi na ya utekelezaji ili kuhakikisha kwamba wananchi—hasa vijana—wanapata nafasi ya kunufaika na uchumi wa buluu.

Wakati huo huo, wamewahimiza vijana wa Pwani kujipanga na kujitolea kwa dhati, ili wawe tayari kutumia fursa zinazojitokeza katika sekta ya uchumi wa bahari kwa manufaa yao binafsi na ya jamii kwa ujumla.

Sekta ya uchumi wa buluu inazidi kutambuliwa kama eneo muhimu la ukuaji wa uchumi, hasa kwa maeneo ya pwani yanayozungukwa na bahari, mito na maziwa makuu.

Continue Reading

Business

Waziri Miano Asisitiza Ushirikiano Kati ya Serikali na Sekta Binafsi Katika Kuimarisha Utalii

Published

on

Waziri wa Utalii, Bi Rebecca Miano, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi katika kuandaa mpango wa pamoja wa kusaidia biashara na maeneo ya utalii nchini.

Akizungumza na wanahabari, Waziri Miano alisema kuwa sekta ya utalii nchini bado inakumbwa na changamoto mbalimbali, hivyo kuna haja ya kuweka mikakati madhubuti ili kuiimarisha na kuiwezesha kuchangia zaidi kwenye uchumi wa taifa.

Aidha, Waziri huyo alieleza kuwa kuna umuhimu wa kuwa na mfumo bora wa kudhibiti na kuboresha ubora wa huduma zinazotolewa katika sekta ya utalii. Alisema mfumo huo unapaswa kuzingatia pia mabadiliko ya tabianchi, ambayo kwa sasa yanaathiri pakubwa shughuli za utalii duniani.

Bi Miano alihitimisha kwa kusema kuwa kwa kuwepo kwa ushirikiano thabiti kati ya pande zote, sekta ya utalii inaweza kuwa chombo kikuu cha kukuza uchumi na kutoa ajira kwa maelfu ya Wakenya.

Continue Reading

Trending