Connect with us

Business

Wafanyabiashara wa Matunda Malindi Walalamikia Kudorora kwa Biashara Kutokana na Ukosefu wa Soko

Published

on

Wafanyabiashara wa kuuza matunda karibu na soko la Kwa Jiwa mjini Malindi, Kaunti ya Kilifi, wanalalamikia kushuka kwa biashara yao kutokana na uhaba wa wateja katika eneo hilo.

Akizungumza na mwanahabari wetu, Mshauri Mkuu wa chama cha Matunda Sales Group, Nathaniel Menza Chengo, amesema kuwa matunda yao yanaendelea kuharibika kila siku kwa kukosa wanunuzi, hali ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kudorora kwa biashara zao.

“Kwa sasa matunda ni mengi lakini hakuna soko. Tunapata hasara kubwa kwa sababu matunda yanaharibika kabla hatujayauza,” amesema Chengo.

Chengo ameitaka serikali ya kitaifa pamoja na serikali ya Kaunti ya Kilifi kuchukua hatua za haraka kwa kujenga kiwanda cha kusindika matunda ili kuwawezesha kuuza bidhaa zao kupitia viwandani. Anasema hatua hiyo itasaidia kupunguza hasara na kuinua maisha ya wafanyabiashara katika eneo hilo.

Amebainisha kuwa kwa sasa, zaidi ya tani 10 za matunda huharibika kila siku kutokana na ukosefu wa soko la uhakika.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Serikali Yalazimika Kufutilia Mbali Deni la Shilingi Bilioni 6 Kutoka Hazina ya Hustler

Published

on

Serikali sasa inasema italazimika kufuta deni la takriban shilingi bilioni 6 kutoka kwa Hazina ya Hustler, baada ya waliopewa mikopo kushindwa kulipa.

Katibu wa Idara ya Biashara Ndogo na za Kati, Bi Susan Mang’eni, amesema juhudi za kuwasaka waliokopa kisha kutotoroka na fedha hizo hazijazaa matunda, licha ya kuwa ni zaidi ya miaka miwili tangu kuanzishwa kwa hazina hiyo.

Kwa mujibu wa Mang’eni, ni Wakenya milioni 10 waliochukua mikopo lakini hawajarejesha, huku milioni 9 kati ya watu milioni 25 waliopokea fedha hizo wakilipa mikopo yao kama inavyotakiwa.

Ameeleza kuwa hali hiyo imeathiri kwa kiasi kikubwa uendelevu wa hazina hiyo, ambayo ililenga kuwainua wananchi kiuchumi kupitia uwezeshaji wa biashara ndogondogo.

Kutokana na hali hiyo, serikali sasa inawasihi wabunge kupitisha ombi la kutengewa shilingi bilioni 5 zaidi katika bajeti ya mwaka huu, ili kuendeleza shughuli za hazina hiyo.

Continue Reading

Business

Wafanyabiashara waomba kufunguliwa kwa soko la Matano Mane, Kaunti ya Kilifi

Published

on

Wafanyabiashara katika soko la Matano Mane, eneo bunge la Vitengeni, Kaunti ya Kilifi, wameiomba serikali ya kaunti kufungua soko la eneo hilo lililojengwa miaka 15 iliyopita lakini hadi sasa halijaanza kutumika.

Wakizungumza na Coco FM, wafanyabiashara hao wamesema kuwa wanakumbwa na changamoto nyingi, hasa wakati huu wa mvua, ambapo bidhaa zao zinaharibiwa kwa kunyeshewa kutokana na ukosefu wa sehemu ya kudumu ya kufanyia biashara.

Josphat Karisa, mmoja wa wafanyabiashara katika soko hilo, amesema kuwa wanalazimika kufanya biashara katika mazingira magumu licha ya kuwepo kwa soko lililojengwa lakini halijafunguliwa rasmi kwa matumizi.

“Tunapitia hasara kubwa wakati huu wa mvua. Bidhaa zetu zinaharibika kwa sababu hatuna mahali pa kudumu pa kufanyia biashara, ilhali kuna soko limejengwa miaka 15 iliyopita lakini halitumiki,” amesema Karisa.

Ameitaka serikali ya Kaunti ya Kilifi kuchukua hatua za haraka kuhakikisha soko hilo linafunguliwa ili wafanyabiashara waweze kuendeleza shughuli zao bila usumbufu na kujikimu kimaisha.

Continue Reading

Trending