Connect with us

Business

Serikali Yalazimika Kufutilia Mbali Deni la Shilingi Bilioni 6 Kutoka Hazina ya Hustler

Published

on

Serikali sasa inasema italazimika kufuta deni la takriban shilingi bilioni 6 kutoka kwa Hazina ya Hustler, baada ya waliopewa mikopo kushindwa kulipa.

Katibu wa Idara ya Biashara Ndogo na za Kati, Bi Susan Mang’eni, amesema juhudi za kuwasaka waliokopa kisha kutotoroka na fedha hizo hazijazaa matunda, licha ya kuwa ni zaidi ya miaka miwili tangu kuanzishwa kwa hazina hiyo.

Kwa mujibu wa Mang’eni, ni Wakenya milioni 10 waliochukua mikopo lakini hawajarejesha, huku milioni 9 kati ya watu milioni 25 waliopokea fedha hizo wakilipa mikopo yao kama inavyotakiwa.

Ameeleza kuwa hali hiyo imeathiri kwa kiasi kikubwa uendelevu wa hazina hiyo, ambayo ililenga kuwainua wananchi kiuchumi kupitia uwezeshaji wa biashara ndogondogo.

Kutokana na hali hiyo, serikali sasa inawasihi wabunge kupitisha ombi la kutengewa shilingi bilioni 5 zaidi katika bajeti ya mwaka huu, ili kuendeleza shughuli za hazina hiyo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wadau wa Sekta ya Uchumi wa Baharini Waisihi Serikali Kuongeza Uwekezaji Pwani

Published

on

Wadau katika sekta ya uchumi wa raslimali za baharini na maziwa katika eneo la Pwani wameitaka serikali kuongeza uwekezaji katika sekta hiyo ili kusaidia kuongeza nafasi za ajira kwa vijana wa eneo hilo.

Kwa mujibu wa wadau hao, serikali haijatoa kipaumbele cha kutosha kwa sekta hiyo, licha ya kuwepo kwa raslimali nyingi za bahari ambazo bado hazijatumika ipasavyo. Wamesisitiza kuwa uwekezaji wa kimkakati unaweza kufungua fursa nyingi kwa vijana, na hivyo kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira katika ukanda wa Pwani.

Viongozi hao pia wameitaka serikali, kupitia wizara husika, kuweka mikakati ya wazi na ya utekelezaji ili kuhakikisha kwamba wananchi—hasa vijana—wanapata nafasi ya kunufaika na uchumi wa buluu.

Wakati huo huo, wamewahimiza vijana wa Pwani kujipanga na kujitolea kwa dhati, ili wawe tayari kutumia fursa zinazojitokeza katika sekta ya uchumi wa bahari kwa manufaa yao binafsi na ya jamii kwa ujumla.

Sekta ya uchumi wa buluu inazidi kutambuliwa kama eneo muhimu la ukuaji wa uchumi, hasa kwa maeneo ya pwani yanayozungukwa na bahari, mito na maziwa makuu.

Continue Reading

Business

Waziri Miano Asisitiza Ushirikiano Kati ya Serikali na Sekta Binafsi Katika Kuimarisha Utalii

Published

on

Waziri wa Utalii, Bi Rebecca Miano, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi katika kuandaa mpango wa pamoja wa kusaidia biashara na maeneo ya utalii nchini.

Akizungumza na wanahabari, Waziri Miano alisema kuwa sekta ya utalii nchini bado inakumbwa na changamoto mbalimbali, hivyo kuna haja ya kuweka mikakati madhubuti ili kuiimarisha na kuiwezesha kuchangia zaidi kwenye uchumi wa taifa.

Aidha, Waziri huyo alieleza kuwa kuna umuhimu wa kuwa na mfumo bora wa kudhibiti na kuboresha ubora wa huduma zinazotolewa katika sekta ya utalii. Alisema mfumo huo unapaswa kuzingatia pia mabadiliko ya tabianchi, ambayo kwa sasa yanaathiri pakubwa shughuli za utalii duniani.

Bi Miano alihitimisha kwa kusema kuwa kwa kuwepo kwa ushirikiano thabiti kati ya pande zote, sekta ya utalii inaweza kuwa chombo kikuu cha kukuza uchumi na kutoa ajira kwa maelfu ya Wakenya.

Continue Reading

Trending