Connect with us

Sports

Rashford Kujiunga na Barcelona Kuimarisha Safu ya Ushambuliaji

Published

on

Mchezaji nyota wa Manchester United, Marcus Rashford, sasa yupo sokoni na anapatikana kwa vilabu vyote kwa ada ya uhamisho ya takriban pauni milioni 40.

Tetesi zinasema kwamba, klabu ya Barcelona bado inaendelea kumfuatilia mshambuliaji huyo, ikiwa ni mwendelezo wa nia waliyoonyesha tangu mwezi Januari mwaka huu.

Hapo awali, dili hilo halikukamilika kutokana na kutokuwepo kwa uuzwaji wa mchezaji mwingine ambaye angewezesha uhamisho huo.

Hivi karibuni, mwandishi wa soka Toni Juanmartí (@tjuanmarti) ameripoti kuwa wawakilishi wa Rashford wamekutana tena na viongozi wa Barcelona kwa mazungumzo zaidi kuhusu uwezekano wa uhamisho huo.

Rashford ametajwa kuwa miongoni mwa wachezaji wanne waliopo kwenye orodha ya Barcelona, wanaochunguzwa kwa ajili ya kuimarisha kikosi hicho msimu ujao.

Ingawa bado hakuna uthibitisho rasmi kuhusu mafanikio ya mazungumzo hayo, uwezekano wa Rashford kujiunga na Barcelona bado upo wazi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

INZAGI Bado Yuko Saana Inter.

Published

on

By

Uongozi wa klabu ya Inter Milan uko radhi kurefusa mkataba wa kocha Simone Inzaghi licha ya kufeli
kutwaa taji la klabu bingwa Uropa siku ya jumamosi.
Rais wa Inter Giuseppe Marotta, ameelezea Imani kwa uongozi wa Kocha Inzaghi, licha ya kibano cha
magoli 5-0 klabu hiyo ilipokea katika fainali ya klabu bingwa uropa dhidi ya Paris Saint-Germain
(PSG) na kupoteza fainali ya pili mtawalia, ya kwanza ikiwa msimu wa mwaka 2022/2023 mikononi
mwa Manchester City.
Mkataba wa Inzaghi unakamilika mwezi juni mwaka ujao ila Marotta, amesisitiza kuwa mazungumzo na
kocha huyo yataanza hivi karibuni, baada ya tetesi kuwa Inzaghi anajiondoa Inter na hatakuwepo
kuitayarisha kwa ajili ya msimu ujao.
“Kushindwa katika fainali hauna msukumo wowote, inzaghi ana mkataba wa mwaka mmoja Zaidi na
tuliamua kukutana naye juma hili” Alisema Marotta katika kikao na wanahabari baada ya fainali ya klabu
bingwa uropa huko Munich Ujerumani. “Mafanikio yote na makali ya klabu yanayoonekana ni kwa ajili
ya uwezo na utaalam wake,Tutafurahia iwapo yuko radhi kuendelea na kazi.”

Continue Reading

Sports

Inter Wapiga Msamba, PSG Wakivuma Uefa.

Published

on

By

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ndio mabingwa wa Klabu bingwa Uropa baada ya kuilaza Inter-Milan magoli 5-0 Jumamosi usiku, katika fainali iliyochezewa katika uwanja wa Allianz Arena jijini Munich, Ujerumani.

Mvua ya magoli ilianzishwa na beki Ashram Hakimi dakika ya 12, kabla ya kiungo mshambuliaji wa PSG Desire Doue kuongeza bao la pili dakika ya 20, na goli la tatu katika dakika ya 60 huku goli la nne na tano likifungwa katika dakika ya 73 na 86 mtawalia.

Kocha wa PSG Luis Enrique amewasifia wachezaji wake sawa na mashabiki waliojitokeza kuishangilia klabu hiyo, ikijipatia taji kuu la kwanza Uropa baada ya kuingia fainali ya mashindano haya mara mbili kwa kipindi cha miaka mitano.

“Nafurahia sana ushindi huu” Alisema Kocha Enrique. “Fainali imekua na hisia sana hasa nilipoona bango la mashabiki kuhusu familia yangu”

Kikosi hichi changa cha PSG kimeafikia kile ambacho wachezaji nyota kama Lionell Messi, Neymar, Zlatan Ibrahimovich, Beckam na Kylian Mbappe walishindwa kutekeleza wakivalia jezi ya PSG

Paris Saint-Germain (PSG) imekua klabu ya pili Ufaransa kushinda taji la Klabu bingwa Uropa baada ya Marseille mwaka 1993.

Continue Reading

Trending