Sports
Rashford Kujiunga na Barcelona Kuimarisha Safu ya Ushambuliaji

Mchezaji nyota wa Manchester United, Marcus Rashford, sasa yupo sokoni na anapatikana kwa vilabu vyote kwa ada ya uhamisho ya takriban pauni milioni 40.
Tetesi zinasema kwamba, klabu ya Barcelona bado inaendelea kumfuatilia mshambuliaji huyo, ikiwa ni mwendelezo wa nia waliyoonyesha tangu mwezi Januari mwaka huu.
Hapo awali, dili hilo halikukamilika kutokana na kutokuwepo kwa uuzwaji wa mchezaji mwingine ambaye angewezesha uhamisho huo.
Hivi karibuni, mwandishi wa soka Toni Juanmartí (@tjuanmarti) ameripoti kuwa wawakilishi wa Rashford wamekutana tena na viongozi wa Barcelona kwa mazungumzo zaidi kuhusu uwezekano wa uhamisho huo.
Rashford ametajwa kuwa miongoni mwa wachezaji wanne waliopo kwenye orodha ya Barcelona, wanaochunguzwa kwa ajili ya kuimarisha kikosi hicho msimu ujao.
Ingawa bado hakuna uthibitisho rasmi kuhusu mafanikio ya mazungumzo hayo, uwezekano wa Rashford kujiunga na Barcelona bado upo wazi.
News
Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.
Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.
Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.
Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.
Sports
Alexander Trent Arnold Sasa Ni Mali Ya Madrid

Kilabu ya Real Madrid imtangaza kupata sahihi ya beki wa taifa la Uingereza na kilabu ya Liverpool Alexander Trent Arnold.
Miamba hao wa Uhispania inaaminika imelipa kima cha Euro milioni 10 kupata sahihi ya beki huyo ambaye amechezea Liverpool tangu utotoni akitokea kwenye academia ya kilabu hiyo.
Trent mwenye umri wa miaka 26 ametia wino mkataba wa miaka sita kilabuni humo inayomueka hadi mwaka 2031.
Makubaliano hayo yakiwa pia kwamba kilabu ya Madrid italipa mshahara wake wa miezi za June na Julai.
Mchezaji huyo anatarajiwa kuvalia jezi la Los Blancos kwa mara ya kwanza katika fainali ya kombe la Dunia baina ya vilabu mwezi ujao Juni 14.