Sports
Mujinga Kutoshiriki Mashindano ya Kipkeino Classic

Mwanariadha nyota kutoka Uswisi, Mujinga Kambundji, hatashiriki katika mashindano ya Kipkeino Classic yanayotarajiwa kufanyika Jumamosi, Mei 31 katika uwanja wa michezo wa Ulinzi, jijini Nairobi.
Kupitia ujumbe alioweka kwenye ukurasa wake wa Instagram Ijumaa iliyopita, Kambundji amethibitisha kuwa hatashiriki tena katika mashindano ya msimu huu wa riadha. Ameeleza kuwa sababu ya kusitisha msimu wake ni ujauzito, na ameahidi kurejea tena uwanjani mwaka ujao.
Kwenye taarifa yake Mujinga alisema, “Msimu umeisha, kwa sababu nzuri zaidi. Nina furaha sana kuwajulisha kuwa muujiza wetu mdogo uko njiani.” Kauli hiyo iliambatana na picha yake akionyesha matokeo ya uchunguzi wa ultrasound, ambao hutumika kuangazia maendeleo ya fetusi na tathmini ya ujauzito.
View this post on Instagram
Kambundji, mwenye umri wa miaka 32, ni mshindi wa medali za dunia mara kadhaa, ikiwa ni pamoja na medali ya shaba katika mashindano ya dunia ya riadha pamoja na mafanikio kwenye mashindano ya ndani ya baridi. Ametangaza kuwa anatarajia kurejea tena kwenye mashindano mwaka wa 2026.
Awali, mashindano ya Kipkeino Classic yalipangwa kufanyika katika uwanja wa Nyayo, lakini kutokana na ukarabati unaoendelea, yamehamishiwa katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex
Sports
INZAGI Bado Yuko Saana Inter.

Uongozi wa klabu ya Inter Milan uko radhi kurefusa mkataba wa kocha Simone Inzaghi licha ya kufeli
kutwaa taji la klabu bingwa Uropa siku ya jumamosi.
Rais wa Inter Giuseppe Marotta, ameelezea Imani kwa uongozi wa Kocha Inzaghi, licha ya kibano cha
magoli 5-0 klabu hiyo ilipokea katika fainali ya klabu bingwa uropa dhidi ya Paris Saint-Germain
(PSG) na kupoteza fainali ya pili mtawalia, ya kwanza ikiwa msimu wa mwaka 2022/2023 mikononi
mwa Manchester City.
Mkataba wa Inzaghi unakamilika mwezi juni mwaka ujao ila Marotta, amesisitiza kuwa mazungumzo na
kocha huyo yataanza hivi karibuni, baada ya tetesi kuwa Inzaghi anajiondoa Inter na hatakuwepo
kuitayarisha kwa ajili ya msimu ujao.
“Kushindwa katika fainali hauna msukumo wowote, inzaghi ana mkataba wa mwaka mmoja Zaidi na
tuliamua kukutana naye juma hili” Alisema Marotta katika kikao na wanahabari baada ya fainali ya klabu
bingwa uropa huko Munich Ujerumani. “Mafanikio yote na makali ya klabu yanayoonekana ni kwa ajili
ya uwezo na utaalam wake,Tutafurahia iwapo yuko radhi kuendelea na kazi.”
Sports
Inter Wapiga Msamba, PSG Wakivuma Uefa.

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ndio mabingwa wa Klabu bingwa Uropa baada ya kuilaza Inter-Milan magoli 5-0 Jumamosi usiku, katika fainali iliyochezewa katika uwanja wa Allianz Arena jijini Munich, Ujerumani.
Mvua ya magoli ilianzishwa na beki Ashram Hakimi dakika ya 12, kabla ya kiungo mshambuliaji wa PSG Desire Doue kuongeza bao la pili dakika ya 20, na goli la tatu katika dakika ya 60 huku goli la nne na tano likifungwa katika dakika ya 73 na 86 mtawalia.
Kocha wa PSG Luis Enrique amewasifia wachezaji wake sawa na mashabiki waliojitokeza kuishangilia klabu hiyo, ikijipatia taji kuu la kwanza Uropa baada ya kuingia fainali ya mashindano haya mara mbili kwa kipindi cha miaka mitano.
“Nafurahia sana ushindi huu” Alisema Kocha Enrique. “Fainali imekua na hisia sana hasa nilipoona bango la mashabiki kuhusu familia yangu”
Kikosi hichi changa cha PSG kimeafikia kile ambacho wachezaji nyota kama Lionell Messi, Neymar, Zlatan Ibrahimovich, Beckam na Kylian Mbappe walishindwa kutekeleza wakivalia jezi ya PSG
Paris Saint-Germain (PSG) imekua klabu ya pili Ufaransa kushinda taji la Klabu bingwa Uropa baada ya Marseille mwaka 1993.