Connect with us

Sports

Mujinga Kutoshiriki Mashindano ya Kipkeino Classic

Published

on

Mwanariadha nyota kutoka Uswisi, Mujinga Kambundji, hatashiriki katika mashindano ya Kipkeino Classic yanayotarajiwa kufanyika Jumamosi, Mei 31 katika uwanja wa michezo wa Ulinzi, jijini Nairobi.

Kupitia ujumbe alioweka kwenye ukurasa wake wa Instagram Ijumaa iliyopita, Kambundji amethibitisha kuwa hatashiriki tena katika mashindano ya msimu huu wa riadha. Ameeleza kuwa sababu ya kusitisha msimu wake ni ujauzito, na ameahidi kurejea tena uwanjani mwaka ujao.

Kwenye taarifa yake Mujinga alisema, “Msimu umeisha, kwa sababu nzuri zaidi. Nina furaha sana kuwajulisha kuwa muujiza wetu mdogo uko njiani.” Kauli hiyo iliambatana na picha yake akionyesha matokeo ya uchunguzi wa ultrasound, ambao hutumika kuangazia maendeleo ya fetusi na tathmini ya ujauzito.

 

View this post on Instagram

 

A post shared by Mujinga Kambundji (@mujingakambundji)

Kambundji, mwenye umri wa miaka 32, ni mshindi wa medali za dunia mara kadhaa, ikiwa ni pamoja na medali ya shaba katika mashindano ya dunia ya riadha pamoja na mafanikio kwenye mashindano ya ndani ya baridi. Ametangaza kuwa anatarajia kurejea tena kwenye mashindano mwaka wa 2026.

Awali, mashindano ya Kipkeino Classic yalipangwa kufanyika katika uwanja wa Nyayo, lakini kutokana na ukarabati unaoendelea, yamehamishiwa katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Mancity Inamnyemelea Kiungo Tijjani Reijnders

Published

on

By

Kilabu ya Manchseter City iko kwenye mazungumzo ya moja kwa moja na kiungo wa AC Milani Tijjani Reijnders kumleta ugani Etihad msimu ujao.

Mawakala wa mchezaji huyo wanataka kitita cha pauni milioni 60 kumwachilia mholanzi huyo ambaye amefunga magoli 19 katika mechi 104 ambazo amechezea Milan

Hata hivyo city wako tayari kutoa pauni milioni 55 kupata sahihi yake  na kumpa kandarasi nono mkataba wa miaka mitano ugani Etihad.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alijiunga na Milan msimu jana akitokea AZ Alkamar ya Eredivise.

City wangali sokoni kupata mrithi wa kiungo mbunifu Kevin De Bruyne ambaye ameondoka kwenye kilabu hiyo baada ya mafanikio makubwa ikidaiwa pia wanamfukuzia kiungo wa Lyon Ryan Cherki raia wa Ufaransa.

Continue Reading

Sports

Arsenal Mbioni Kumpata Mshambulizi Sesko

Published

on

By

Kilabu ya Arsenal imeambiwa ni lazima itoe kitita cha pauni milioni 75 kunasa huduma za mshambulizi wa taifa la Slovenia na kilabu ya RB Leipzig Benjamin Sesko.

Inaaminika na The Gunners kupitia kwa Afisa mkuu mtendaji Andrea Berta wamekua na mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa mchezaji huyo na pia afisa wa Leipzig Marcel Schafer kuhusiana matakwa ya uhamisho huo.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 alikua na magoli 21 msimu huu akichangia mengine sita katika michezo yote alizoshirikisha akiwa miongoni mwa wafungaji bora ligi ya Bundesliga nchini Ujerumani.

The Gunners wako sokoni kusaka mshambulizi atakayewapa taji msimu ujao huku ikidaiwa pia watafanya mazungumzo na mshambulizi wa Sporting Lisbon Victor Gyokeres ambaye alifunga zaidi ya magoli 40 msimu ambao umekamilika.

Continue Reading

Trending