Connect with us

Sports

Arsenal Karibu Kufikia Makubaliano Mapya na Beki Gabriel

Published

on

Klabu ya Arsenal ipo katika hatua za mwisho za mazungumzo na beki wao wa kati, Gabriel Magalhães, kuhusu mkataba mpya.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 raia wa Brazil, bado ana mkataba unaoendelea hadi mwaka 2027, lakini klabu hiyo imekuwa ikijadiliana naye kuhusu masharti mapya ya kuboresha mkataba huo.

Ikumbukwe kuwa mazungumzo hayo yamepiga hatua kubwa, na makubaliano yanaelekea kukamilika hivi karibuni.

Taarifa hiyo inakuja kama faraja kubwa kwa The Gunners wakati wanajiandaa kwa msimu wa uhamisho wa majira ya joto, ambapo wanatarajiwa kufanya usajili muhimu ili kuimarisha kikosi.

Gabriel amekuwa mchezaji wa msingi chini ya kocha Mikel Arteta, ingawa msimu wake ulimalizika mapema mwezi Aprili kufuatia majeraha ya paja yaliyomlazimu kufanyiwa upasuaji.

Hata hivyo, beki huyo anatarajiwa kuwa fiti kabla ya msimu mpya kuanza.

Katika msimu uliomalizika wa mwaka 2024/2025, Gabriel alifunga magoli matano katika mashindano yote akiwa na Arsenal.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

INZAGI Bado Yuko Saana Inter.

Published

on

By

Uongozi wa klabu ya Inter Milan uko radhi kurefusa mkataba wa kocha Simone Inzaghi licha ya kufeli
kutwaa taji la klabu bingwa Uropa siku ya jumamosi.
Rais wa Inter Giuseppe Marotta, ameelezea Imani kwa uongozi wa Kocha Inzaghi, licha ya kibano cha
magoli 5-0 klabu hiyo ilipokea katika fainali ya klabu bingwa uropa dhidi ya Paris Saint-Germain
(PSG) na kupoteza fainali ya pili mtawalia, ya kwanza ikiwa msimu wa mwaka 2022/2023 mikononi
mwa Manchester City.
Mkataba wa Inzaghi unakamilika mwezi juni mwaka ujao ila Marotta, amesisitiza kuwa mazungumzo na
kocha huyo yataanza hivi karibuni, baada ya tetesi kuwa Inzaghi anajiondoa Inter na hatakuwepo
kuitayarisha kwa ajili ya msimu ujao.
“Kushindwa katika fainali hauna msukumo wowote, inzaghi ana mkataba wa mwaka mmoja Zaidi na
tuliamua kukutana naye juma hili” Alisema Marotta katika kikao na wanahabari baada ya fainali ya klabu
bingwa uropa huko Munich Ujerumani. “Mafanikio yote na makali ya klabu yanayoonekana ni kwa ajili
ya uwezo na utaalam wake,Tutafurahia iwapo yuko radhi kuendelea na kazi.”

Continue Reading

Sports

Inter Wapiga Msamba, PSG Wakivuma Uefa.

Published

on

By

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ndio mabingwa wa Klabu bingwa Uropa baada ya kuilaza Inter-Milan magoli 5-0 Jumamosi usiku, katika fainali iliyochezewa katika uwanja wa Allianz Arena jijini Munich, Ujerumani.

Mvua ya magoli ilianzishwa na beki Ashram Hakimi dakika ya 12, kabla ya kiungo mshambuliaji wa PSG Desire Doue kuongeza bao la pili dakika ya 20, na goli la tatu katika dakika ya 60 huku goli la nne na tano likifungwa katika dakika ya 73 na 86 mtawalia.

Kocha wa PSG Luis Enrique amewasifia wachezaji wake sawa na mashabiki waliojitokeza kuishangilia klabu hiyo, ikijipatia taji kuu la kwanza Uropa baada ya kuingia fainali ya mashindano haya mara mbili kwa kipindi cha miaka mitano.

“Nafurahia sana ushindi huu” Alisema Kocha Enrique. “Fainali imekua na hisia sana hasa nilipoona bango la mashabiki kuhusu familia yangu”

Kikosi hichi changa cha PSG kimeafikia kile ambacho wachezaji nyota kama Lionell Messi, Neymar, Zlatan Ibrahimovich, Beckam na Kylian Mbappe walishindwa kutekeleza wakivalia jezi ya PSG

Paris Saint-Germain (PSG) imekua klabu ya pili Ufaransa kushinda taji la Klabu bingwa Uropa baada ya Marseille mwaka 1993.

Continue Reading

Trending