Sports
Arsenal Karibu Kufikia Makubaliano Mapya na Beki Gabriel

Klabu ya Arsenal ipo katika hatua za mwisho za mazungumzo na beki wao wa kati, Gabriel Magalhães, kuhusu mkataba mpya.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 raia wa Brazil, bado ana mkataba unaoendelea hadi mwaka 2027, lakini klabu hiyo imekuwa ikijadiliana naye kuhusu masharti mapya ya kuboresha mkataba huo.
Ikumbukwe kuwa mazungumzo hayo yamepiga hatua kubwa, na makubaliano yanaelekea kukamilika hivi karibuni.
Taarifa hiyo inakuja kama faraja kubwa kwa The Gunners wakati wanajiandaa kwa msimu wa uhamisho wa majira ya joto, ambapo wanatarajiwa kufanya usajili muhimu ili kuimarisha kikosi.
Gabriel amekuwa mchezaji wa msingi chini ya kocha Mikel Arteta, ingawa msimu wake ulimalizika mapema mwezi Aprili kufuatia majeraha ya paja yaliyomlazimu kufanyiwa upasuaji.
Hata hivyo, beki huyo anatarajiwa kuwa fiti kabla ya msimu mpya kuanza.
Katika msimu uliomalizika wa mwaka 2024/2025, Gabriel alifunga magoli matano katika mashindano yote akiwa na Arsenal.
Sports
Mancity Inamnyemelea Kiungo Tijjani Reijnders

Kilabu ya Manchseter City iko kwenye mazungumzo ya moja kwa moja na kiungo wa AC Milani Tijjani Reijnders kumleta ugani Etihad msimu ujao.
Mawakala wa mchezaji huyo wanataka kitita cha pauni milioni 60 kumwachilia mholanzi huyo ambaye amefunga magoli 19 katika mechi 104 ambazo amechezea Milan
Hata hivyo city wako tayari kutoa pauni milioni 55 kupata sahihi yake na kumpa kandarasi nono mkataba wa miaka mitano ugani Etihad.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alijiunga na Milan msimu jana akitokea AZ Alkamar ya Eredivise.
City wangali sokoni kupata mrithi wa kiungo mbunifu Kevin De Bruyne ambaye ameondoka kwenye kilabu hiyo baada ya mafanikio makubwa ikidaiwa pia wanamfukuzia kiungo wa Lyon Ryan Cherki raia wa Ufaransa.
Sports
Arsenal Mbioni Kumpata Mshambulizi Sesko

Kilabu ya Arsenal imeambiwa ni lazima itoe kitita cha pauni milioni 75 kunasa huduma za mshambulizi wa taifa la Slovenia na kilabu ya RB Leipzig Benjamin Sesko.
Inaaminika na The Gunners kupitia kwa Afisa mkuu mtendaji Andrea Berta wamekua na mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa mchezaji huyo na pia afisa wa Leipzig Marcel Schafer kuhusiana matakwa ya uhamisho huo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 alikua na magoli 21 msimu huu akichangia mengine sita katika michezo yote alizoshirikisha akiwa miongoni mwa wafungaji bora ligi ya Bundesliga nchini Ujerumani.
The Gunners wako sokoni kusaka mshambulizi atakayewapa taji msimu ujao huku ikidaiwa pia watafanya mazungumzo na mshambulizi wa Sporting Lisbon Victor Gyokeres ambaye alifunga zaidi ya magoli 40 msimu ambao umekamilika.