Connect with us

News

Mashahidi zaidi wajitokeza dhidi ya Mackenzie

Published

on

Kesi dhidi ya mhubiri tata Paul Mackenzie na washukiwa wenzake 38 kuhusu ukatili na ukiukaji wa haki za watoto inaendelea kusikizwa katika mahakama ya watoto ya Tononoka, Mombasa mbele ya hakimu mkuu Nelly Chepchirchir.

Shahidi wa 43, Sajenti mwandamizi Joseph Yator, alieleza jinsi mtoto aliyenusurika kutoka Shakahola alivyoripoti kuwa watoto wawili walifunikwa nyuso na mama zao hadi kufariki baada ya kushindwa kufa kwa kufunga.

Yator alisema alipewa amri ya mahakama kufukua miili hiyo ili kubaini chanzo cha vifo hivyo, lakini baada ya Mackenzie kuachiliwa kwa dhamana ya polisi, alikuta makaburi hayo yakiwa matupu.

Aliongeza kuwa mwili mmoja kati ya hiyo miwili ulipatikana kwenye  kaburi tofauti na kupelekwa kwa vipimo vya DNA, ambapo matokeo yalionyesha kufanana kwa asilimia 99 na ndugu wa familia hiyo.

Shahidi wa 44, Julius Kiprotich, alisimulia jinsi mkewe, Alice Kawira, aliyefuata mafundisho ya Mackenzie, alivyochoma vitabu na sare za shule za watoto wao, na pia kumtoa mamake hospitalini na kutupa dawa zake, akidai matibabu ni ushetani.

Kiprotich alitoa ushahidi wa kusikitisha akieleza jinsi mkeke na wafuasi wengine wa kanisa la Good News International walivyosherehekea kifo cha mtoto wao wa pili badala ya kuomboleza, baada ya mkewe kushindwa kumpeleka mtoto hospitalini.

Alieleza mahakama jinsi mkewe alivyomtoa mtoto kwa siri kutoka shule na kuhamia Shakahola na kisha kukatiza mawasiliano.

Mama yake Julius Kiprotich, Bi. Hellena, pia alithibitisha ushahidi  wa mwanawe kwa kueleza kuwa Alice Kawira na Julius walikuwa wanandoa na walikuwa na watoto wawili, ushahidi wake pia uliunga mkono madai ya Julius kwamba Alice Kawira alimtoa mtoto wao shuleni Eldoret na kuhamia Malindi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wataalam wa Uchumi wa Bahari washinikiza Viongozi kuwawezesha Wananchi.

Published

on

By

Wataalamu wa sekta ya uchumi wa samawati na maswala ya bahari hapa nchini wamesistiza haja ya serikali kuweka mazingira bora ya kubuni nafasi zaidi ya ajira ili kuinua uchumi wa bahari.

Mtaalam wa sekta hiyo Stanley Chai alisema uboreshaji wa mazingira ya sekta hiyo utachangia waekezaji zaidi kuekeza hapa nchini.

Chai alidokeza kuwa bahari hindi inafursa kubwa ya kuinua uchumi wa nchi kutokana na raslimali zinazopatikana bahari hindi.

“Nilazima tuweke mazingira yakuvutia meli nyingi, hii bahari yetu kuna mda ukiangalia kuna meli hamsini zinapita, tumekuwa tukishauri ulimwengu na kinachofanyika ni kuweka mazingira ya kuekeza upatikanaji wa samaki wa kiviwanda nchini, kama saa hii Kenya mtu akitaka liseni ya kwenda kuvua samaki kama hivi tuna tunamtoza dola elfu hamusini kwa mwaka”,alisema Chai.

Kuhusu swala la kudhibiti uingizaji wa bidhaa za samaki kutoka taifa la uchina katika soko la hapa nchini, mtaalam huyo alisema uhaba wa samaki hapa nchini umechangia uendelezaji wa biashara baina ya nchi hizo mbili ili kutosheleza lishe miongoni mwa jamii nchini.

 “Japan ndio walaji wakubwa wa samaki ulimwenguni, samaki wakiletwa hapa ndio wavuvi wetu watafaidi, wakati samaki wanapelekwa nje ujue samaki wetu wenye thamani ndio wanaenda nje na sisi tunakula tilapia ambao wameletwa kutoka huko, kama samaki wangekuwa wanatutosheleza hapa hakungekuwa na soko la wachina, lakini kwa sababu hawatutoshelezi ndio maana watu wamepata mwanya wa kuleta”, aliongeza mtaalam huyo.

Mtaalam wa maswala ya uchumi wa bahari Stanley Chai akipokezwa zawadi na Coco fm.

Wakati huo huo alishinikiza viongozi hapa nchini kutafuta ufahamu zaidi kuhusu maswala ya uchumi wa bahari sawa na kuweka mikakati ya kubuni nafasi za ajira ili kuwezesha wananchi kimaendeleo.

“Haieleweki kama wewe ni mbunge unasema utaendeleza eneo bunge lako na CDF ya shilingi milioni 170, hakuna maendeleo utaleta, kwa hivyo vingozi tunafaa kufikiria tofauti, tuje na njia mbadala ya kwamba tutabuni ajira na tutaleta utajiri watu wajitegemee na njia moja rahisi ni hii, sisi tunashukuru sana rais alisikiza akaelewa na kwa mara ya kwanza akaunda wizara nzima ya uchumi samawati, ninini tena unataka? Unataka kumlaumu rais tena?”, aliuliza Chai.

Tamko la mtaalam huyo linajiri wakati Kenya ikiadhimisha sherehe za miaka 62 za siku ya madaraka, ambazo ziliongozwa na rais William Ruto katika kaunti ya Homabay huku kauli mbiu ya maadhimisho ya sherehe za mwaka huu ikiwa ni “Uchumi sanawati na maswala ya bahari”.

Taarifa na Joseph Jira

 

Continue Reading

News

Rais Ruto amewaongoza wakenya kuadhimisha sherehe za Madaraka za 62

Published

on

By

Rais William Ruto amewaongoza wakenya katika kuadhimisha sherehe za Madaraka za 62 tangu taifa lijipatie uhuru.

Katika maadhimisho hayo ambayo yamefanyika katika uwanja wa Raila Odinga kaunti ya Homabay, Rais Ruto amesema taifa limepiga hatua kidemokrasia na maendeleo tangu lijipatie uhuru.

Kiongozi wa taifa ametoa changamoto kwa wakenya kuhakikisha wanaweka kipau mbele masuala ya kutekeleza mabadiliko yanayoleta ufanisi wa Taifa.

Wakenya washeherekea Madaraka, Homabay

Naye Naibu rais Prof Kithure Kindiki amemhakikishia Rais Ruto kuwa ataendelea kushirikiana naye katika kuunganisha taifa huku akimtaja Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga kama kiongozi aliyechangia zaidi mshikamano wa taifa.

Kwa upande wake Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga amemtaka Rais Ruto kuhakikisha serikali inafidia familia za wakenya walipoteza wapendwa wao wakati wa Maandamano ya vijana wa Gen Z mwezi Juni mwaka jana.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya sherehe za mwaka huu ni “uchumi wa sanawati na maswala ya bahari”, huku ikilenga kuangazia fursa za kiuchumi zinazotokana na raslimali ya maji.

Continue Reading

Trending