News
Mashahidi zaidi wajitokeza dhidi ya Mackenzie

Kesi dhidi ya mhubiri tata Paul Mackenzie na washukiwa wenzake 38 kuhusu ukatili na ukiukaji wa haki za watoto inaendelea kusikizwa katika mahakama ya watoto ya Tononoka, Mombasa mbele ya hakimu mkuu Nelly Chepchirchir.
Shahidi wa 43, Sajenti mwandamizi Joseph Yator, alieleza jinsi mtoto aliyenusurika kutoka Shakahola alivyoripoti kuwa watoto wawili walifunikwa nyuso na mama zao hadi kufariki baada ya kushindwa kufa kwa kufunga.
Yator alisema alipewa amri ya mahakama kufukua miili hiyo ili kubaini chanzo cha vifo hivyo, lakini baada ya Mackenzie kuachiliwa kwa dhamana ya polisi, alikuta makaburi hayo yakiwa matupu.
Aliongeza kuwa mwili mmoja kati ya hiyo miwili ulipatikana kwenye kaburi tofauti na kupelekwa kwa vipimo vya DNA, ambapo matokeo yalionyesha kufanana kwa asilimia 99 na ndugu wa familia hiyo.
Shahidi wa 44, Julius Kiprotich, alisimulia jinsi mkewe, Alice Kawira, aliyefuata mafundisho ya Mackenzie, alivyochoma vitabu na sare za shule za watoto wao, na pia kumtoa mamake hospitalini na kutupa dawa zake, akidai matibabu ni ushetani.
Kiprotich alitoa ushahidi wa kusikitisha akieleza jinsi mkeke na wafuasi wengine wa kanisa la Good News International walivyosherehekea kifo cha mtoto wao wa pili badala ya kuomboleza, baada ya mkewe kushindwa kumpeleka mtoto hospitalini.
Alieleza mahakama jinsi mkewe alivyomtoa mtoto kwa siri kutoka shule na kuhamia Shakahola na kisha kukatiza mawasiliano.
Mama yake Julius Kiprotich, Bi. Hellena, pia alithibitisha ushahidi wa mwanawe kwa kueleza kuwa Alice Kawira na Julius walikuwa wanandoa na walikuwa na watoto wawili, ushahidi wake pia uliunga mkono madai ya Julius kwamba Alice Kawira alimtoa mtoto wao shuleni Eldoret na kuhamia Malindi.
News
Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.
Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.
Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.
Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.
News
Shughuli za Masomo Zatatizwa katika Shule ya Msingi ya Arabuko Sokoke

Shughuli za masomo katika shule ya msingi ya Arabuko Sokoke eneo la Kakuyuni kaunti ya Kilifi zilitatizika mapema siku ya Ijumaa baada ya Wazazi kuandamana wakilalamikia usimamizi mbaya wa shule hiyo.
Wakaazi hao wamemtaka Mwalimu kuu wa shule hiyo kupewa uhamisho kwani ameonyesha wazi kushindwa kusimamia shughuli za masomo katika shule hiyo.
Wakiongozwa na Joyce Mbuche, Wazazi hao wamesema Mwalimu mkuu wa shule hiyo amekosa kuwa wazi kwa wazazi kuhusu suala la matumizi ya Fedha ya shule hiyo pamoja na kutokuwa muadilifu kazini.
Wazazi hao hata hivyo wamesema Mwalimu mkuu huyo amekuwa hawalipi mishahara walimu ambao wanasimamiwa na wazazi katika shule hiyo huku baadhi ya wanafunzi wakikosa kusajiliwa katika mfumo wa KEMIS.