Sports
Kilabu ya Chelsea Ndiyo Mabingwa wa Conference League

Kilabu ya Chelsea ya Uingereza imekua ya kwanza kushinda taji la Kilabu Bingwa Ulaya,taji la Uefa Europa ligi,Uefa Supa Cup na Taji la Conference ligi katika historia ya mataji hayo barani Ulaya.
Hii ni baada ya The Blues kutia darasani kabla ya kuchachafya kilabu ya Real Betis ya Uhispania kichapo cha magoli 4-1 uwanjani majeski stadium,Poland fainali ya conference ligi.
Kilabu ya Real Betis walitanguliwa kufunga kupitia winga matata wa taifa la Morocco Abde Elizouzoli dakika ya 9 Lakini chelsea walikua na jambo lao wakirejea kwa kishindo kipindo cha pili kupitia magoli ya kiungo MuArgentina Enzo Fernandez dakika 65,kisha Mshambulizi wa taifa la Senegal Nicholas Jackson akipachika wavuni goli la pili dakika ya 70,
winga matata wa Manchester United Muingereza Jadon Sancho aliongeza la tatu dakika ya 70,huku Kiungo mkabaji Moses Caicedo akizika Betis kwa chuma cha nne kunako dakika ya 93 na kunyakua kombe hilo.
Kombe hilo ni taji la kwanza kwa kocha Enzo Maresca kilabuni humo na hakuficha furaha yake baada ya kuwapa furaha mashabiki wa The Blues.
Sports
Mancity Inamnyemelea Kiungo Tijjani Reijnders

Kilabu ya Manchseter City iko kwenye mazungumzo ya moja kwa moja na kiungo wa AC Milani Tijjani Reijnders kumleta ugani Etihad msimu ujao.
Mawakala wa mchezaji huyo wanataka kitita cha pauni milioni 60 kumwachilia mholanzi huyo ambaye amefunga magoli 19 katika mechi 104 ambazo amechezea Milan
Hata hivyo city wako tayari kutoa pauni milioni 55 kupata sahihi yake na kumpa kandarasi nono mkataba wa miaka mitano ugani Etihad.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alijiunga na Milan msimu jana akitokea AZ Alkamar ya Eredivise.
City wangali sokoni kupata mrithi wa kiungo mbunifu Kevin De Bruyne ambaye ameondoka kwenye kilabu hiyo baada ya mafanikio makubwa ikidaiwa pia wanamfukuzia kiungo wa Lyon Ryan Cherki raia wa Ufaransa.
Sports
Arsenal Mbioni Kumpata Mshambulizi Sesko

Kilabu ya Arsenal imeambiwa ni lazima itoe kitita cha pauni milioni 75 kunasa huduma za mshambulizi wa taifa la Slovenia na kilabu ya RB Leipzig Benjamin Sesko.
Inaaminika na The Gunners kupitia kwa Afisa mkuu mtendaji Andrea Berta wamekua na mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa mchezaji huyo na pia afisa wa Leipzig Marcel Schafer kuhusiana matakwa ya uhamisho huo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 alikua na magoli 21 msimu huu akichangia mengine sita katika michezo yote alizoshirikisha akiwa miongoni mwa wafungaji bora ligi ya Bundesliga nchini Ujerumani.
The Gunners wako sokoni kusaka mshambulizi atakayewapa taji msimu ujao huku ikidaiwa pia watafanya mazungumzo na mshambulizi wa Sporting Lisbon Victor Gyokeres ambaye alifunga zaidi ya magoli 40 msimu ambao umekamilika.