Connect with us

News

Manusua wa Mkasa Baharini, Kilifi

Published

on

Mafisa wa uokoaji kaunti ya Kilifi bado wanaendelea kupiga mbizi baharini kutafuta Mwili wa Mwanabaharia mmoja Kapteni Kivondi, aliyezama Jumamosi usiki wa tarehe 24 Aprili, akiwa na wengine wawili katika mkono wa Bahari mjini Kilifi.

Kapteni Kivondi alifariki pamoja na mwenzake Kapteni Mwidini wakati wa mkasa huo, huku baharia mwengine wa tatu Aisha Jumwa akinusurika baada ya kuogelea baharini kwa zaidi ya masaa 16.

Akizungumza na CocoFm iliyomtembelea Hospitalini mjini Kilifi, Jumwa alielezea matukio hayo wakati mawimbi makali yalipopiga chombo chao na kukizamisha.

Mwili wa baharia mwengine ambaye alikuwa msaidizi wa nahodha wa Dau hilo, Kapteni Mwidini ulipatikana katika ufuo wa Watamu, umbali wa kilomita 50 kutoka mji wa Kilifi. Mwili wa marehemu uliondolewa na kusafirishwa hadi eneo la Likoni Mjini Mombasa kwa Maziko.

Aisha Jumwa -Manusuru wa mkasa wa baharini mjini Kilifi

Jumwa anasema kuwa aliweza kuokolewa siku iliyofuatia ya Jumapili, mwendo was saa sita adhuhuri baada ya kuogelea kwa maasaa hayo 16 licha ya upepo na mawimbi makali yaliyozidi kumsukuma maji makuu.

Kisa hiki kilitokea masaa machache tu hata baada ya idara ya Utabiri wa hali ya hewa kutoa tahadhari ya kuchafuka kwa Bahari na marufuku ya kuepuka fuo za bahari.

Hata hivyo Jumwa anasema kuwa tahadhari hiyo iliwapata kuchelewa hadi mkasa huo ulipowakuta. Anaongeza kwamba baada ya Dau lao kuzama watatu hao walijifunga Kamba ili waweza kuolea na kusaidiana lakini wawili hao wakashindwa na nguvu ya mawimbi hayo makali na kuaga dunia mikononi mwake

Taarifa ya Lolani Kalu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Published

on

By

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.

Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.

Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.

Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.

Continue Reading

News

Shughuli za Masomo Zatatizwa katika Shule ya Msingi ya Arabuko Sokoke

Published

on

By

Shughuli za masomo katika shule ya msingi ya Arabuko Sokoke eneo la Kakuyuni kaunti ya Kilifi zilitatizika mapema siku ya Ijumaa baada ya Wazazi kuandamana wakilalamikia usimamizi mbaya wa shule hiyo.

Wakaazi hao wamemtaka Mwalimu kuu wa shule hiyo kupewa uhamisho kwani ameonyesha wazi kushindwa kusimamia shughuli za masomo katika shule hiyo.

Wakiongozwa na Joyce Mbuche, Wazazi hao wamesema Mwalimu mkuu wa shule hiyo amekosa kuwa wazi kwa wazazi kuhusu suala la matumizi ya Fedha ya shule hiyo pamoja na kutokuwa muadilifu kazini.

Wazazi hao hata hivyo wamesema Mwalimu mkuu huyo amekuwa hawalipi mishahara walimu ambao wanasimamiwa na wazazi katika shule hiyo huku baadhi ya wanafunzi wakikosa kusajiliwa katika mfumo wa KEMIS.

Continue Reading

Trending