Connect with us

News

Kenya Kuandaa Mashindano Ya Karate JKA Mwaka 2027

Published

on

Kenya imechaguliwa kuandaa mashindano ya mchezo wa Karate wa mabingwa barani Africa wa shirikisho la Japan Karate Association JKA mwaka 2027.
Hii ni mara ya kwanza kabisa mchezo huo kuandaliwa nje ya ardhi ya Africa Kusini.
Rais wa shirikisho la JKA nchini Kenya Wakili George Kithi anasema, hii ni heshima kubwa kwa Kenya kuwa mwenyeji wa mashindano hayo ya kimatifa, na kuongeza Kwamba ni dhihirisho mchezo huu unazidi kupata umaarufu sio tu kwa mashabiki wa Karate nchini Kenya, bali kote barani Africa.

Rais wa shirikisho la mchezo wa karate la Japan Karate Association (JKA) nchini Kenya Wakili George Kithi akiwa na kikosi cha Kenya katika ukumbi wa Ellis Park mjini Johannesberg, Afrika Kusini baada ya kukamilika kwa mashindano ya mwaka huu.

Wakili Kithi anasema, hii itakuwa fursa nzuri Kenya kuonyesha umahiri wake wa kuandaa mashindano ya kimatifa lakini pia kukuza vipawa na kuitangaza Kenya kama kituo Bora Cha Utalii.
Hii inafuatia ushindi mkubwa wakati wa mashindano yaliyokamilika hivi majuzi nchini Africa Kusini ambapo Kenya ilimaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Africa Kusini.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Published

on

By

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.

Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.

Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.

Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.

Continue Reading

News

Shughuli za Masomo Zatatizwa katika Shule ya Msingi ya Arabuko Sokoke

Published

on

By

Shughuli za masomo katika shule ya msingi ya Arabuko Sokoke eneo la Kakuyuni kaunti ya Kilifi zilitatizika mapema siku ya Ijumaa baada ya Wazazi kuandamana wakilalamikia usimamizi mbaya wa shule hiyo.

Wakaazi hao wamemtaka Mwalimu kuu wa shule hiyo kupewa uhamisho kwani ameonyesha wazi kushindwa kusimamia shughuli za masomo katika shule hiyo.

Wakiongozwa na Joyce Mbuche, Wazazi hao wamesema Mwalimu mkuu wa shule hiyo amekosa kuwa wazi kwa wazazi kuhusu suala la matumizi ya Fedha ya shule hiyo pamoja na kutokuwa muadilifu kazini.

Wazazi hao hata hivyo wamesema Mwalimu mkuu huyo amekuwa hawalipi mishahara walimu ambao wanasimamiwa na wazazi katika shule hiyo huku baadhi ya wanafunzi wakikosa kusajiliwa katika mfumo wa KEMIS.

Continue Reading

Trending