Connect with us

News

Vijana wa Kaunti ya Kilifi Wajisajili kwa Kazi za Ughaibuni

Published

on

Mamia ya vijana wamejitokeza katika uwanja wa Karisa Maitha mjini Kilifi Kaunti ya Kilifi kutafuta usajili wa kazi za ughaibuni kama ilivyotangazwa na serikali.

Kulingana na serikali, eneo la Pwani limetengewa nafasi 3,500 za kazi za ughaibuni katika mpango wa ajira uliopewa jina “Kazi Majuu” ikiwepo kazi za kuendesha piki piki, ubawabu, vijakazi shambani pamoja na wahudumu nyumbani.

Wengi wa vijana waliojitokeza katika zoezi hilo wameeleza matumaini ya kubadili maisha yao iwapo watafanikiwa, wakidai maisha ya humu nchini yamezidi kuwa magumu.

Kulingana na Jilani Justin Mwarumba mmoja wa vijana hao wameasema serikali inafaa kuwahakikishia usalama wa pesa watakazotumia katika zoezi hilo huku wakishinikiza kuangazia upya suala la ulipaji mkopo kwa wasio na uwezo wa kugharamia zoezi hilo la usajali.

Hata hivyo Wanaharakati wa kijamii mjini Kilifi wakiongozwa na Birya Menza wanashinikiza serikali kuhakikisha inabuni nafasi za ajira hapa nchini badala ya mataifa ya ugaibuni ambako wakenya wengi wamekuwa wakipitia madhila mengi mikononi mwa waajiri.

Zoezi hilo litaendelea katika kaunti zaMombasa na Kwale.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto Awaomba Radhi Watanzania.

Published

on

By

Rais William Ruto amejitokeza na kuomba msamaha kwa niaba ya vijana wa Gen Z dhidi ya utawala wa Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Rais Ruto ameisihi serikali ya Tanzania kuondoa hofu kuhusu Mabishano makali ya Mtandaoni baina ya mataifa  haya mawili  licha ya Viongozi wa mataifa haya mawili Rais William Ruto na Mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan  kuonekana kujaribu kuuzima moto wa mashambulio ya mitandaoni hasa miongoni mwa vijana wa Gen Z.

Akizungumza wakati wa dhifa ya asubuhi ya maombi ya kitaifa yaliondaliwa jijini Nairobi, Rais Ruto amesema kuna haja ya kuendeleza ushirikiano mwema wa kidiplomasia na wala sio kuchangia uhasama, akiwaomba msamaha pia vijana wakenya.

Viongozi wahudhuria dhifa ya asubuhi ya maombi ya kitaifa

Kauli ya Rais Ruto imejiri baada Bunge la Tanzania kulazimika  kusitisha vikao vya kawaida na kujadili hoja inayotajwa kugusia usalama wa taifa la Tanzania huku wakimpongeza rais Samia Suluhu Hassan kwa hatua aliyochukua ya kuwafurusha Wanaharakati  wa kutetea haki za binadamu wakiongozwa na Martha Karua ambaye kiongozi wa chama cha People’s Liberation Party nchini Kenya na Jaji Mkuu mstaafu Willy Mutunga, Mwanaharakati Boniface Mwangi wa Kenya na Agather Atuhaire wa Uganda.

Mwanaharakati Bonifance Mwangi alipatikana  katika eneo la mpakani mwaka Kenya na Tanzania katika eneo la Lunga lunga ilihali mwenzake  Agather Atuhaire akipatikana karibu na kituo cha mpakani na Mtukula.

Continue Reading

News

Manusua wa Mkasa Baharini, Kilifi

Published

on

By

Mafisa wa uokoaji kaunti ya Kilifi bado wanaendelea kupiga mbizi baharini kutafuta Mwili wa Mwanabaharia mmoja Kapteni Kivondi, aliyezama Jumamosi usiki wa tarehe 24 Aprili, akiwa na wengine wawili katika mkono wa Bahari mjini Kilifi.

Kapteni Kivondi alifariki pamoja na mwenzake Kapteni Mwidini wakati wa mkasa huo, huku baharia mwengine wa tatu Aisha Jumwa akinusurika baada ya kuogelea baharini kwa zaidi ya masaa 16.

Akizungumza na CocoFm iliyomtembelea Hospitalini mjini Kilifi, Jumwa alielezea matukio hayo wakati mawimbi makali yalipopiga chombo chao na kukizamisha.

Mwili wa baharia mwengine ambaye alikuwa msaidizi wa nahodha wa Dau hilo, Kapteni Mwidini ulipatikana katika ufuo wa Watamu, umbali wa kilomita 50 kutoka mji wa Kilifi. Mwili wa marehemu uliondolewa na kusafirishwa hadi eneo la Likoni Mjini Mombasa kwa Maziko.

Aisha Jumwa -Manusuru wa mkasa wa baharini mjini Kilifi

Jumwa anasema kuwa aliweza kuokolewa siku iliyofuatia ya Jumapili, mwendo was saa sita adhuhuri baada ya kuogelea kwa maasaa hayo 16 licha ya upepo na mawimbi makali yaliyozidi kumsukuma maji makuu.

Kisa hiki kilitokea masaa machache tu hata baada ya idara ya Utabiri wa hali ya hewa kutoa tahadhari ya kuchafuka kwa Bahari na marufuku ya kuepuka fuo za bahari.

Hata hivyo Jumwa anasema kuwa tahadhari hiyo iliwapata kuchelewa hadi mkasa huo ulipowakuta. Anaongeza kwamba baada ya Dau lao kuzama watatu hao walijifunga Kamba ili waweza kuolea na kusaidiana lakini wawili hao wakashindwa na nguvu ya mawimbi hayo makali na kuaga dunia mikononi mwake

Taarifa ya Lolani Kalu

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.