News
Polisi wamewakamata vijana sita Wahalifu, Kaunti ya Kilifi.

Maafisa wa Idara ya DCI kwa ushirikiano na kitengo maalum cha Polisi wamefanikiwa kuwakamata vijana sita wanaoshukiwa kuwa wahalifu.
Katika taarifa ya Polisi, wahalifu nao wanadaiwa kwamba wamekuwa wakiwapora wananchi fedha zao wanapozuru benki mbalimbali.
Kamanda wa Polisi eneo la Kilifi Kusini Hassan Rochale amethibitisha kukamatwa kwa wahalifu hao, akisema maafisa wa polisi wako makini kuhakikisha wahalifu wote wanakabiliwa kisheria.
Maafisa wa polisi wamesema wakati wa makabiliano na wahalifu hao, mhalifu mmoja alipigwa risasi na kujeruhiwa mkono huku magari mawili yenye nambari bandia za usajali pamoja na vifaa nyingine hatari vilivyotumika kwa uhalifu vikinaswa na maafisa wa polisi.
Aidha wamesema wahalifu hao wamekuwa wakiwahangaisha wakaazi wa kaunti za Kilifi na Mombasa, na kwamba wamekamatwa katika eneo la Kadzengo kwenye barabara kuu ya Mombasa – Malindi wakielekea maeneo ya Mtwapa kutoka Kilifi.
Wahalifu hao ni pamoja na Erick Wachira, Ali Said Nassir, Fredrick Kalugo Konde, Nicholas Mungaro Kitumba, Fred Mwajira, na Edwin Kyalo Mulandi.
Wahalifu hao wanazuiliwa katika kituo cha polisi cha Kijipwa kaunti ya Kilifi wakisubiri kufikishwa Mahakamani.
News
Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.
Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.
Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.
Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.
News
Shughuli za Masomo Zatatizwa katika Shule ya Msingi ya Arabuko Sokoke

Shughuli za masomo katika shule ya msingi ya Arabuko Sokoke eneo la Kakuyuni kaunti ya Kilifi zilitatizika mapema siku ya Ijumaa baada ya Wazazi kuandamana wakilalamikia usimamizi mbaya wa shule hiyo.
Wakaazi hao wamemtaka Mwalimu kuu wa shule hiyo kupewa uhamisho kwani ameonyesha wazi kushindwa kusimamia shughuli za masomo katika shule hiyo.
Wakiongozwa na Joyce Mbuche, Wazazi hao wamesema Mwalimu mkuu wa shule hiyo amekosa kuwa wazi kwa wazazi kuhusu suala la matumizi ya Fedha ya shule hiyo pamoja na kutokuwa muadilifu kazini.
Wazazi hao hata hivyo wamesema Mwalimu mkuu huyo amekuwa hawalipi mishahara walimu ambao wanasimamiwa na wazazi katika shule hiyo huku baadhi ya wanafunzi wakikosa kusajiliwa katika mfumo wa KEMIS.