Connect with us

News

Mapato ya Wavuvi hapa Kilifi yameongezeka

Published

on

Mwenyekiti wa muungano wa wahudumu wa maboti kaunti ya Kilifi Shallo Issa maarufu captain Shallo amesema kuwa mapato ya wavuvi msimu huu yameongezeka ikilinganishwa na hapo awali.

Katika mazungumzo ya kipekee yaCoco fm, captain Shallo amesema  kuwa wavuvi wote wanaotumia vifaa vya hali ya juu sawa na wale wavuvi wadogowadogo wameimarika kimapato muda huu.

Shallo amesema kuwa wavuvi hao wamekuwa wakiuza samaki kwa wingi sio tu hapa Kilifi lakini pia kwenye kaunti nyinginezo za Kenya sawa na taifa jirani la Tanzania.

Wakati huohuo Shallo amedokeza kuwa rais William Ruto kupitia wizara ya uchumi na raslimali za baharini na maziwa, analenga kuweka sehemu tatu ambazo zitajengwa bandari ndogo katika kaunti hii ya Kilifi.

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Published

on

By

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.

Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.

Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.

Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.

Continue Reading

News

Shughuli za Masomo Zatatizwa katika Shule ya Msingi ya Arabuko Sokoke

Published

on

By

Shughuli za masomo katika shule ya msingi ya Arabuko Sokoke eneo la Kakuyuni kaunti ya Kilifi zilitatizika mapema siku ya Ijumaa baada ya Wazazi kuandamana wakilalamikia usimamizi mbaya wa shule hiyo.

Wakaazi hao wamemtaka Mwalimu kuu wa shule hiyo kupewa uhamisho kwani ameonyesha wazi kushindwa kusimamia shughuli za masomo katika shule hiyo.

Wakiongozwa na Joyce Mbuche, Wazazi hao wamesema Mwalimu mkuu wa shule hiyo amekosa kuwa wazi kwa wazazi kuhusu suala la matumizi ya Fedha ya shule hiyo pamoja na kutokuwa muadilifu kazini.

Wazazi hao hata hivyo wamesema Mwalimu mkuu huyo amekuwa hawalipi mishahara walimu ambao wanasimamiwa na wazazi katika shule hiyo huku baadhi ya wanafunzi wakikosa kusajiliwa katika mfumo wa KEMIS.

Continue Reading

Trending