Connect with us

News

Kilabu Ya Arsenal Yaboronga Uefa

Published

on

Uefa

Kilabu ya PSG ya Ufaransa kucheza dhidi ya Inter ya Italia kwenye fainali ya uefa baada ya kunyamazisha kabla ya kuzimisha kilabu ya Arsenal kipigo cha magoli 2-1 ugani Parc de prince siku ya jumatano.

Kiungo wa Uhispania Fabain Ruiz aliwaweka uongozini Psg kunako dakika ya 27 kabla ya Akraf Hakimi kuweka la pili kunako dakika 72 kipindi cha pili ikawa ni jumla ya magoli 3-1

Goli la kufutia machozi la Arsenal lilitiwa kimyani ni winga wa Uingereza Bukayo Saka kunako dakika ya 76 kipindi cha pili na kuzamisha kabisa matumaini ya timu kupata taji msimu huu.

Hata hivyo baada ya kubanduliwa nje kocha wa The Gunners Mikel Arteta angali na asisitiza walikua timu bora kwenye kombe hilo huku akidai Psg walisadiwa pakubwa na kipa wao Gianluigi Donnaruma raia wa Italia aliyefanya kazi kubwa ya makombozi na kuwanyima nafasi vijana wake.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wanaosajiliwa Kwenye Mpango wa Kazi “Majuu” Waonywa.

Published

on

By

Waziri wa Leba nchini Dakta Alfred Mutua amewaonya vijana waliopata nafasi za ajira ughaibuni dhidi ya kujihusisha na visa vya utovu wa nidhamu.

Akizungumza wakati wa zoezi la kusajili vijana kwenye mpango wa ajira za nje nchi maarufu Kazi “Majuu” katika kaunti ya Kwale, Waziri Mutua alitaja hatua hiyo kwamba huenda ikachangia kandarasi zao kufutiliwa mbali sawa na kukabiliwa kisheria.

Mutua alidokeza kwamba kuna baadhi ya vijana ambao tayari wamerejeshwa nchini kufuatia visa vya utovu wa nidhamu

“Unaskia unawashwa unataka kuandamana, unataka kuwa mwanaharakati, unataka kuchochea ingia ndege uje hapa wikendi moja uandamane kila mahali hiyo kitu ikutoke urejee kazini, kwa sababu ukienda kufanya huko maandamano unaharibia wakenya wengine, kuna watu waliandamana huko nchi tofauti tofauti, wakenya kumi na tano wengi wakasimamishwa, wakaregeshwa nyumbani, unaandamana kwa nchi nyengine wanauliza mbona mkenya anaandamana na mganda haandamani, mbona mtanzania haandamani”, alisema waziri Mutua.

Akizungumzia suala la utumizi wa dawa za kulevya, Waziri Mutua amewataka vijana hao kukomesha uraibu huo kwani  hakuna taifa linaloshabikia matumizi ya dawa za kulevya.

“Hapa utafanyia ukaguzi wa kiafya kama umekuwa ukivuta bangi, madawa ya kulevya utaanguka, hata ukikataa kupatikana hapa ukifika ng’ambo  utapatikana, kwa hivyo kama unataka kwenda ng’ambo achana na bangi bwana”,aliongeza waziri Mutua.

Zoezi hilo lililenga vijana 800 kaunti ya Kwale na 3,500 eneo la pwani kwa ujumla.

Taarifa ya Joseph Jira

 

 

 

Continue Reading

News

Waasi wa M23 wazidisha Mapambano, DRC

Published

on

By

Mapigano mapya yamezuka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo baada ya Waasi wa kundi la M23 kufutilia mbali pendekezo la ahadi za hapo awali za kujiondoa katika maeneo wanayoyadhibiti huku wakilishtumu jeshi la Kongo kwa kuendeleza uchokozi.

Wakati hayo yakiarifiwa, mataifa jirani yanaendelea kijaribu kufufua mchakato wa kutafuta amani katika taifa hilo ambalo limetumbukia katika migogogo ya kiutawala. Inaarifiwa kwamba Watu wawili wameuawa kufuatia mashambulio yaliyotokea katika hafla ya Mazishi ya Mwanamuziki maarufu wa Kongo.

Waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda katika maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanapambana na waasi wanaoegemea upande wa serikali huku nchi za kikanda zikijaribu kuupa msukumo mpya mchakato wa kutafuta amani ambao umekuwa ukisuasua.

 Waasi wa M23 wamefanikiwa kuiteka miji miwili mikubwa mashariki mwa Kongo tangu Januari huku maelfu ya vifo vikiripotiwa na mamia ya maelfu ya watu wakilazimika kuyakimbia makazi yao.

Mapigano hayo yanazidi kupamba moto licha ya juhudi za viongozi  wa nchi za ukanda wa Kusini mwa Mashariki mwa Africa kuutanzua Mgogoro huo unaotishia kusambaa na kuwa vita vikubwa vya kikanda.

Taarifa ya Eric Ponda.  

Continue Reading

Trending