News
Tiketi za Mashemeji Debi Zimeanza Kuuzwa

Debi la mashemeji kati ya mahasimu wa tangu jadi kilabu ya Gor Mahia na Afc leopards siku ya jumapili kuendelea kama ilivyopangwa haya ni kwa mujibu wa waandalilizi wa mtananga huo Gor.
Tiketi za mchuano huo tayari zimetolewa ambapo mashabiki wa kawaida wanalipia ada ya shilingi shs.300 na mashabiki mashuhuri shs.500.
Awali kulikua na hali ya sintofahamu kuhusiana na ubora wa uwanja wa Kasarani ambao bado unakarabatiwa kuanda mechi ila wakilishi wa kogalo wamepata hakikisho kutoka kwa wasimamizi wa uga huo.
Katika mechi ya mkondo wa kwanza timu hizo mbili ziliisha sare tasa ugani Nyayo,Kogalo kwa sasa ni ya tatu ligini na alama 51 huku Afc Leoprads wakiwa ya sita na alama 42 kutokana na mechi 29.
News
Rais Ruto Awaomba Radhi Watanzania.

Rais William Ruto amejitokeza na kuomba msamaha kwa niaba ya vijana wa Gen Z dhidi ya utawala wa Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.
Rais Ruto ameisihi serikali ya Tanzania kuondoa hofu kuhusu Mabishano makali ya Mtandaoni baina ya mataifa haya mawili licha ya Viongozi wa mataifa haya mawili Rais William Ruto na Mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuonekana kujaribu kuuzima moto wa mashambulio ya mitandaoni hasa miongoni mwa vijana wa Gen Z.
Akizungumza wakati wa dhifa ya asubuhi ya maombi ya kitaifa yaliondaliwa jijini Nairobi, Rais Ruto amesema kuna haja ya kuendeleza ushirikiano mwema wa kidiplomasia na wala sio kuchangia uhasama, akiwaomba msamaha pia vijana wakenya.
Viongozi wahudhuria dhifa ya asubuhi ya maombi ya kitaifa
Kauli ya Rais Ruto imejiri baada Bunge la Tanzania kulazimika kusitisha vikao vya kawaida na kujadili hoja inayotajwa kugusia usalama wa taifa la Tanzania huku wakimpongeza rais Samia Suluhu Hassan kwa hatua aliyochukua ya kuwafurusha Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu wakiongozwa na Martha Karua ambaye kiongozi wa chama cha People’s Liberation Party nchini Kenya na Jaji Mkuu mstaafu Willy Mutunga, Mwanaharakati Boniface Mwangi wa Kenya na Agather Atuhaire wa Uganda.
Mwanaharakati Bonifance Mwangi alipatikana katika eneo la mpakani mwaka Kenya na Tanzania katika eneo la Lunga lunga ilihali mwenzake Agather Atuhaire akipatikana karibu na kituo cha mpakani na Mtukula.
News
Manusua wa Mkasa Baharini, Kilifi

Mafisa wa uokoaji kaunti ya Kilifi bado wanaendelea kupiga mbizi baharini kutafuta Mwili wa Mwanabaharia mmoja Kapteni Kivondi, aliyezama Jumamosi usiki wa tarehe 24 Aprili, akiwa na wengine wawili katika mkono wa Bahari mjini Kilifi.
Kapteni Kivondi alifariki pamoja na mwenzake Kapteni Mwidini wakati wa mkasa huo, huku baharia mwengine wa tatu Aisha Jumwa akinusurika baada ya kuogelea baharini kwa zaidi ya masaa 16.
Akizungumza na CocoFm iliyomtembelea Hospitalini mjini Kilifi, Jumwa alielezea matukio hayo wakati mawimbi makali yalipopiga chombo chao na kukizamisha.
Mwili wa baharia mwengine ambaye alikuwa msaidizi wa nahodha wa Dau hilo, Kapteni Mwidini ulipatikana katika ufuo wa Watamu, umbali wa kilomita 50 kutoka mji wa Kilifi. Mwili wa marehemu uliondolewa na kusafirishwa hadi eneo la Likoni Mjini Mombasa kwa Maziko.
Aisha Jumwa -Manusuru wa mkasa wa baharini mjini Kilifi
Jumwa anasema kuwa aliweza kuokolewa siku iliyofuatia ya Jumapili, mwendo was saa sita adhuhuri baada ya kuogelea kwa maasaa hayo 16 licha ya upepo na mawimbi makali yaliyozidi kumsukuma maji makuu.
Kisa hiki kilitokea masaa machache tu hata baada ya idara ya Utabiri wa hali ya hewa kutoa tahadhari ya kuchafuka kwa Bahari na marufuku ya kuepuka fuo za bahari.
Hata hivyo Jumwa anasema kuwa tahadhari hiyo iliwapata kuchelewa hadi mkasa huo ulipowakuta. Anaongeza kwamba baada ya Dau lao kuzama watatu hao walijifunga Kamba ili waweza kuolea na kusaidiana lakini wawili hao wakashindwa na nguvu ya mawimbi hayo makali na kuaga dunia mikononi mwake
Taarifa ya Lolani Kalu