Connect with us

News

Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta awataka vijana barani afrika kudumisha amani

Published

on

Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta ametoa wito kwa vijana katika bara hili la afrika kuwa katika mstari wa mbele katika kuhakikisha kwamba kuna umoja kwenye bara hili.

Kenyatta ambaye alikuwa akizungumza katika Kongamano la kila mwaka la viongozi wa vyama kwenye chuo kikuu cha Makere nchini Uganda amesema kuna umuhimu wa vijana kuchukua nafasi yao katika jamii na kuliongoza bara hili la Afrika.

Aidha, Kenyatta amesema vijana wana mchango mkubwa zaidi katika kuliimarisha bara hili na kusisitiza hoja ya kuondolewa kwa vikwazo vya kibiashara baina ya mataifa ya bara la Afrika ili kuimarisha sekta hiyo.

Picha kwa hisani | Rais mstaafu Uhuru Kenyatta akisalimiana na rais wa Uganda Yoweri Kaguta Mseveni

Vilevile, Kenyatta ametoa wito kwa wadau mbalimbali barani Afrika kuendelea kuangazia uvumbuzi kama njia mojawapo ya kuimarisha maisha ya vijana ili kuwaepusha na vishawishi ambavyo vinaweza kuwafanya kupotoka kimaadili.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.

Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.

Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.

Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.

Continue Reading

News

Amref, yaikabidhi kaunti ya Kilifi vifaa ya matibabu vya milioni 13.2

Published

on

By

Shirika la Afya la AMREF kwa ushirikiano na serikali ya kaunti ya Kilifi wawekeza zaidi katika sekta ya afya ili kukabiliana na magonjwa yaliyosaulika.

Shirika hilo limeikabidhi serikali ya kaunti ya Kilifi vifaa vya matibabu vya thamani ya shilingi milioni 13.2 ili kuwawezesha wahudumu wa afya kutathmini magonjwa mbalimbali yaliyosaulika na kuboresha sekta ya afya mashinani.

Mkurugenzi wa Shirika la Afya la AMREF humu nchini Daktari Ndirangu Wanjuki, amesema vifaa hivyo vitasaidia katika kubaini magonjwa yaliyosaulika kama vile Kichocho na kuwawezesha wahudumu wa afya kuwahuhudumia wagonjwa ipasavyo.

Akizungumza wakati wa halfa ya kupokea vifaa hiyo katika hospitali kuu ya rufaa ya Kilifi, Gavana wa kaunti Kilifi Gedion Mung’aro amesema vifaa hiyo vitasambazwa katika hospitali na zahanati 15 za kaunti hiyo.

Gavana Mung’aro amesema magonjwa kama vile Kichocho na Matende miongoni mwa wagonjwa mengine yatagunduliwa kwa urahisi na kutibiwa kwani mengi husababishwa na viini kwenye maji machafu hasa kandokando ya mito.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.