Connect with us

News

Maelfu ya Watu Wapeana Heshima ya Mwisho kwa Papa Francis

Published

on

Maelfu ya Waumini wa Kanisa katoliki kote ulimwenguni wamepata fursa ya kupeyana heshima yao ya mwisho kwa mwendazake Papa Francis katika Kanisa Katoliki la St. Peters Basilica mjini Vatican.

Mwili wa Papa Francis utasalia katika Kanisa hilo kwa siku tatu kwa ajili ya waumini kuutazama huku maombi maalum yakiendelea kabla ya halfa ya mazishi siku ya Jumamosi Aprili 26 baada ya Misa ya Ibada ya wafu mjini Vatican.

Kabla ya waumini kuruhusiwa kuutazama mwili wa Papa, Kadinali Kevin Farrell ameongoza ibada maalum mapema leo asubuhi baada ya mwili wa Papa kutolewa katika makaazi yake ya Casa Santa Marta hadi Kanisa la St Peters Basilica ukiwa katika jeneza lililo wazi

Maelfu ya waumini wa Kanisa Katoliki wamewasili mjini Vatican kutoa heshima yao ya mwisho kwa mwendazake Papa Francis aliyefariki dunia mnamo siku ya Jumatatu Aprili 21 baada ya kuugua kiharusi.

Viongozi wa mataifa mbalimbali ulimwenguni wakiongozwa na Rais wa Marekani Donald Trump wanatarajiwa kuhudhuria ibada hiyo ya wafu siku ya Jumamosi, kabla ya mazishi katika Kanisa la Mary Major, nje ya Kanisa la St Peters Basilica.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

News

Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.

Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.

Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.

Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.