News
Maelfu ya Watu Wapeana Heshima ya Mwisho kwa Papa Francis

Maelfu ya Waumini wa Kanisa katoliki kote ulimwenguni wamepata fursa ya kupeyana heshima yao ya mwisho kwa mwendazake Papa Francis katika Kanisa Katoliki la St. Peters Basilica mjini Vatican.
Mwili wa Papa Francis utasalia katika Kanisa hilo kwa siku tatu kwa ajili ya waumini kuutazama huku maombi maalum yakiendelea kabla ya halfa ya mazishi siku ya Jumamosi Aprili 26 baada ya Misa ya Ibada ya wafu mjini Vatican.
Kabla ya waumini kuruhusiwa kuutazama mwili wa Papa, Kadinali Kevin Farrell ameongoza ibada maalum mapema leo asubuhi baada ya mwili wa Papa kutolewa katika makaazi yake ya Casa Santa Marta hadi Kanisa la St Peters Basilica ukiwa katika jeneza lililo wazi
Maelfu ya waumini wa Kanisa Katoliki wamewasili mjini Vatican kutoa heshima yao ya mwisho kwa mwendazake Papa Francis aliyefariki dunia mnamo siku ya Jumatatu Aprili 21 baada ya kuugua kiharusi.
Viongozi wa mataifa mbalimbali ulimwenguni wakiongozwa na Rais wa Marekani Donald Trump wanatarajiwa kuhudhuria ibada hiyo ya wafu siku ya Jumamosi, kabla ya mazishi katika Kanisa la Mary Major, nje ya Kanisa la St Peters Basilica.
News
Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.
Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.
Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.
Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.
Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.
News
Amref, yaikabidhi kaunti ya Kilifi vifaa ya matibabu vya milioni 13.2

Shirika la Afya la AMREF kwa ushirikiano na serikali ya kaunti ya Kilifi wawekeza zaidi katika sekta ya afya ili kukabiliana na magonjwa yaliyosaulika.
Shirika hilo limeikabidhi serikali ya kaunti ya Kilifi vifaa vya matibabu vya thamani ya shilingi milioni 13.2 ili kuwawezesha wahudumu wa afya kutathmini magonjwa mbalimbali yaliyosaulika na kuboresha sekta ya afya mashinani.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya la AMREF humu nchini Daktari Ndirangu Wanjuki, amesema vifaa hivyo vitasaidia katika kubaini magonjwa yaliyosaulika kama vile Kichocho na kuwawezesha wahudumu wa afya kuwahuhudumia wagonjwa ipasavyo.
Akizungumza wakati wa halfa ya kupokea vifaa hiyo katika hospitali kuu ya rufaa ya Kilifi, Gavana wa kaunti Kilifi Gedion Mung’aro amesema vifaa hiyo vitasambazwa katika hospitali na zahanati 15 za kaunti hiyo.
Gavana Mung’aro amesema magonjwa kama vile Kichocho na Matende miongoni mwa wagonjwa mengine yatagunduliwa kwa urahisi na kutibiwa kwani mengi husababishwa na viini kwenye maji machafu hasa kandokando ya mito.