Connect with us

News

Murkomen, Awaonya Maafisa wa Mahakama Dhidi ya Ufisadi

Published

on

Kutokana na kushuhudiwa kwa mizozo ya ardhi ya mara kwa mara katika eneo la Pwani, sasa Wizara ya Usalama wa ndani imewaonya maafisa wa idara ya Mahakama katika kaunti ya Kilifi kukoma kuchochea mizozo ya ardhi.

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen, amesema tabia hiyo inafaa kukomeshwa na maafisa wa idara ya Mahakama kuzingatia haki ya kila mmoja wakati wanapotoa agizo lolote kuhusu suala tata la ardhi kwa wakaazi wa kaunti ya Kilifi.

Akizungumza mjini Kilifi wakati wa kikao cha jukwaa la usalama, Waziri Murkomen amesema atafanya mazungumzo na Jaji mkuu nchini Martha Koome kuhusu suala hilo tata ili kuhakikisha maafisa wa idara ya Mahakama ambao wanajihusisha na ufisadi na unyakuzi wa ardhi wanakabiliwa kisheria.

Murkomen amesema sheria imeeleza wazi kwamba mtu yeyote akiishi katika ardhi kwa zaidi ya miaka 12 bila ya usumbufu wowote basi ana haki ya kisheria kupewa hati miliki ya ardhi hiyo, akisisitiza kwamba mizozo ya ardhi Pwani itapata suluhu hivi karibuni.

Wakati huo huo amedokeza kwamba tayari Wizara ya usalama wa ndani, ile ya ardhi nchini, viongozi wa kisiasa pamoja na wadau mbalimbali wanaendelea na mikakati bora ya kuhakikisha suala tata la ardhi kanda ya Pwani linapata suluhu la kudumu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

News

Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.

Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.

Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.

Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.