Connect with us

News

Askofu Lagho: Marufuku Siasa Kanisani

Published

on

Askofu wa Kanisa Katoliki jimbo mkuu la Malindi Willybard Lagho, ametoa onyo kali kwa viongozi wa kisiasa dhidi ya kutumia vibaya Kanisa na kuendeleza maswala ya kisiasa na utakatishaji fedha.

Askofu Lagho amesema Kanisa hilo halitakubali viongozi wa kisiasa kulitumia vibaya kwa manufaa yao binafsi, akisisitiza haja ya wanasiasa kuheshimu sehemu za Ibada.

Katika taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari, Askofu Lagho amesema mwanasiasa yeyote atakayemujulisha kiongozi wa kanisa kuhusu mipango yake na ibada maalum atakazoshiriki Kanisani hafai kutambulishwa Kanisani.

Askofu Lagho amewaonya mapadre na viongozi wa makanisa katoliki katika jimbo kuu la Malindi kwamba watachukuliwa hatua za kinidhamu iwapo watakosa kuzingatia agizo hilo la Kanisa.

Wakati huo huo amesema Kanisa halikatazi mtu kushiriki ibada Kanisani bali halitakubali baadhi ya watu wenye ushawishi pamoja na wanasiasa kutumia vibaya sehemu za Ibada.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Published

on

By

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.

Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.

Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.

Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.

Continue Reading

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.