News
Wafanyikazi wa Vibarua Katika Hospitali ya Mariakani Wameanza Mgomo Baridi

Wafanyikazi wa vibarua katika Hospitali ya Mariakani kaunti ya Kilifi wameanza mgomo baridi wakilalamikia usimamizi duni wa hospitali hiyo sawa na kukosa kulipwa mishahara yao kwa kipindi cha miezi miwili.
Wakiongozwa na Mwenyekiti wao Rajab Juma Mumo, wafanyikazi hao wa vibarua wamesema kumekuwa na sintofahamu katika ulipaji mishahara kwani licha ya wafanyikazi hao kuwa zaidi ya 70 ni wafanyikazi 40 pekee watakaopewa kandarasi na kampeni binafsi.
Mumo amelalakia kutojumuishwa kwa wafanyikazi hao katika mikataba mipya ya uajiri sawa na kutopewa mishahara yao kwa kipindi cha miezi miwili kutoka kwa usimamizi wa hospitali hiyo pamoja na serikali ya kaunti ya Kilifi.
Aidha wamesema wamefanya kazi katika Hospitali hiyo ikiwemo kusafisha mazingira miongoni mwa kazi zengine kwa zaidi ya miaka sita bila ya kupewa ajira za kudumu.
Hata hivyo juhudi za Wanahabari wetu kubaini uhalali wa madai hayo ziligonga mwamba kwani wasimamizi wa hospitali hiyo sawa na viongozi kutoka serikali ya kaunti ya Kilifi wamekataa kuzungumzia swala hilo.
News
Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.
Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.
Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.
News
Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.
Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.
Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.