Sports
Makala ya mbio za magari WRC kufikia Tamati Jumapili Hii

Maelfu ya mashabiki kutoka afrika mashariki na kati wamiminika mjini Naivasha kaunti ya Nakuru kwa mbio za magari ya WRC Makala ya mwaka 2025.
Kwa mujibu wa waandalizi Zaidi ya mashabiki 30,000 wametua jijini humo kutoka mataifa ya Uganda,Tanzania na Rwanda kwa mbio hizo ambazo zilianza rasmi siku ya alhamisi jijini Nairobi.
Eflyn Evans dereva kutoka taifa la Wales ndio anaongeza akitumia gari aina ya Toyota Gazoo muda sekunde 46.1 baada ya raundi ya pili akifuatwa na bingwa mara mbili Kalle Rovanpera raia wa uhispania akitumia Toyota pia watatu ni Ottok Tanak raia wa Estonia ambaye anatumia gari aina ya Hyundai Shell Mobis.
Dereva anayeongoza mpaka sasa dereva Eflyn Evans na msaidizi wake Scott Martin alikua na haya yakusema baada ya kuchukua uongozi wa mapmea.
“Plan yetu ilifanya kazi vizuri,tunafuraha kuchukua uongozi wa mapema ila bado kazi ipo kwani mizungumzo ni minane,tutaona itakavyokua mpaka siku ya mwisho.”
Kwa upande wake dereva nambari mbili na bingwa mtetezi Kalle Rovanpera na msaidizi wake Jonne Halttunen alisema haya baada ya kushindwa;
“Leo haikua siku nzuri kwetu tulitumia muda mwingi asubuhi ila bado safari ya sisi kurejea kileleni.”
Naye dereva namba tatu Ott Tanak aliyasema haya;
“Hauwezi ukapanga kusema kweli ukiwa hapa kenya vitu vingi vinafanyika,Ni lazima tuketi chini tufahamu tatizo ambalo linatukumba na gari letu.”
Raundi ya tatu na nne yanaishwa maeneo ya Elmentaita huku jumapili mbio hizo zikiisha Hells Gate 1 na Hells GATE 2.
Kilele cha mbio hizo ni siku ya jumapili ambapo rais William Samoei Ruto anatarajiwa kufunga mbio hizo.
News
Liverpool Kutangazwa Bingwa Mpya Epl

Miamba wa Uingereza kilabu ya Liverpool kutangazwa mabingwa wapya wa ligi kuu EPL Wikendi hii iwapo watatoka sare ya aina yoyote dhidi ya kilabu ya Tottenham Hotspurs ugani Anfield.
Haya yanajiri baada ya kilabu nambari mbili Arsenal kudondosha alama mbili muhimu siku ya jumatano dhidi ya Crystal Place timu hizo zikiisha sare ya magoli 2-2 uwanjani Emirates na kudidimiza matumaini yake ya kutwaa ubingwa wa Epl msimu huu.
Beki Jacob Kiwior aliweka uongozini The Gunners kunako dakika 3 kabla ya Palace kusawazisha kupitia kwa kiungo mshmabulizi Eze Oberechi kunako dakika ya 22 na licha ya kuchukua uongozi mwingine kupitia Leandro Trossard dakika ya 46,kilabu ya Palace ilijibu dakika ya 84 kupitia kwa mshambulizi Jean Philip Mateta.
Matokeo haya yanawacha Liverpool nafasi ya kwanza na alama 79 nayo Arsenal nafasi ya pili na alama 67 nayo mancity wakiwa nafasi ya tatu na alama 61 nayo Nottingham Forest ni ya nne na alama 60 mkiani ni vilabu vya Ipwisch Town,Leicester city na Southampton mtawalia.
News
Matokeo Yataanza Kuja Tu

Mkufunzi wa kilabu ya kiifi united Samson Jumbe amesema kwamba ana Imani vijana wake watarejea katika hali ya kupata matokeo chanya licha ya vijana wake kupoteza mechi 2 mfululizo ikiwemo debi kati yao na kilabu ya United Brothers mwishoni mwa jumwa
Kwa mujibu wa mwalimu huyo kwa sasa wanalenga kuimarisha safu yao ya mashambulizi ambayo imekua ikipoteza nafasi nyingi za wazi.
“Naamini kwa uwezo wa mwenyezi Mungu vijana wangu wataanza kufunga magoli na kuanza kushinda mechi za ligi ya kaunti kuanzia wikendi hii nyumbani,mechi ya tumecheza vizuri kasoro magoli tu.”
Kwa upande wake kocha wa kilabu ya united Brothers Titus Kitaka amesema kwamba mazoezi mazito ambayo amekua na vijana wake imewasaidia pakubwa kupata matokeo mazuri tangu ligi hiyo kungoa nanga.
“Sisi ni ushindi tu kwa sababu tufanye mazoezi ya kutosha kwa ajili ya ligi hii ya kaunti na malengo yetu yanasalia pale pale kushinda na kupanda msimu ujao.”
Kilifi United inaketi nafasi ya 9 na imepoteza mechi mbili mfululizo kati nne ambazo wamecheza huku United Brothers wakishinda tatu na kupoteza moja pekee.