Connect with us

National News

Marekani Yatoa Tahadhari ya Usafiri kwa Raia wake, Kenya

Published

on

TAHADHARI-

Taifa la Marekani limetoa tahadhari ya usafiri kwa raia wake, likiwataka kutotembelea maeneo ya mpaka wa Kenya na Somalia kutokana uwezekano wa kutokea mashambulizi ya kigaidi, uhalifu na utekejinyara.

 

Kupitia Ubalozi wake humu nchini, taifa hilo limetaja kaunti za Mandera, Wajir na Garissa kama maeneo hatari yenye matukio ya kigaidi na kuwashauri raia wake kutotembelea sehemu hizo.

Katika ukanda wa Pwani, ubalozi huo wa Marekani umewatahadharisha raia wake dhidi ya kutembelea maeneo kadhaa ya kaunti ya Kilifi ikiwemo Kaskazini mwa mji wa Malindi na kaunti ya Lamu na Tana River.

Tahadhari hiyo hata hivyo haikutaja mbuga ya kitaifa ya wanyama ya Tsavo, japo ikafahamisha kaunti za West Pokot na Turkana kama kaunti ambazo ziko katika hatari kutokana na matukio ya uvamizi wa majangili wanaoiba mifugo.

Wakati uo huo Marekani imetahadharisha raia wake kuwa makini wanapotembelea sehemu za Kibera na Eastleigh jijini Nairobi kutokana na ongezeko la visa vya uhalifu ambavyo vimekuwa vikichangia changamoto kwa maafisa wa usalama kuvikabili.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Chonga: Wakenya Wanaosafiri Ughaibuni Kusaka Ajira Hawazingatii Sheria za Leba

Published

on

By

Mwenyekiti wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa Ken Chonga amesema baadhi ya wakenya ambao wanasafiri katika mataifa ya miliki za kiarabu kusaka ajira wamekosa kuzingatia sheria za Wizara ya Leba nchini na kuangukia mikononi mwa walaghai.

Chonga amesema ni lazima wakenya hao wachunguze mawakala wanaowasafirisha katika mataifa hayo kama wanatambulika na serikali, ndipo waingie katika mikataba ya uajiri ambayo imezingatia sheria za Leba nchini.

Akizungumza na Wanahabari mjini Kilifi, Chonga ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kusini amesema ili wakenya waepuke madhila mbalimbali kutoka kwa waajiri wao katika mataifa hayo ni lazima wasafirishwe na mawakala waliosajiliwa na serikali.

Wakati huo huo amesema japo serikali iko mbioni kuhakikisha inawatafutia wakenya kazi katika mataifa ya ughaibuni ni lazima wanaosaka ajira za ughaibuni waingie katika mkataba wa uajiri kabla ya kusafiri nje ya nchi.

Continue Reading

National News

Chibule: Visa vya Dhulma za Kijinsi Vimepungua Kilifi

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imesema visa vya dhulma za kijinsia katika kaunti hiyo vimepungua kwa kiwango kikubwa.

Kulingana na Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Mbetsa Chibule, visa hivyo viliongezeka zaidi msimu wa maambukizi ya virusi vya Corona, ambapo kaunti ya Kilifi iliorodheswa nafasi ya tatu nchini baada ya kaunti ya Bungoma na Samburu.

Chibule amesema kwa sasa ni asilimia 12.3 pekee ya visa hivyo vilivyoripotiwa tofauti na asilimia 30 wakati wa maambukizi ya Corona, akisisitiza kwamba juhudi hizo zimefanikiwa kupitia ushirikiano wa jamii na wadau mbalimbali.

Kiongozi huyo amedokeza kwamba serikali ya kaunti imetoa mafunzo kwa maafisa wa kutoa ushauri nasaha ili kusaidia kupambana na visa hivyo mashinani, akisema juhudi hizo zitaendelezwa sawa na kudhibiti madhila hayo.

Wakati uo huo ameweka wazi kwamba kaunti hiyo imekamilisha ujenzi wa sehemu salama ya kuwahifadhi watoto wanaopitia dhulma za kijinsia wakati kesi zao zikiendelea Mahakamani.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.