National News
Wanaotafuta Nafasi ya Mwenyekiti wa IEBC Kuhojiwa Jumatatu

Jopo la uteuzi wa Makamishna wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC limetangaza kuanza zoezi la kuwapigwa msasa watu 11 ambao walituma maombi ya kujaza nafasi ya Mwenyeti wa Tume ya IEBC.
Joto hilo limetoa orodha ya zoezi hilo, kwamba siku ya Jumatatu tarehe 24 mwezi huu wa Machi, watakaohojiwa ni pamoja na aliyekuwa msajili mkuu wa idara ya Mahakama nchini Anne Amadi, aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya utekelezaji Katiba CIC Chalse Nyachae, Edward Katama kutoka TransNzoia na Abdulqudir Lorot kutoka Baringo.
Mwengine ni pamoja na Erastus Edung Ethekon, Francis Kakai Kissinger, Joy Brenda Masinde-Mdivo, Jacob Ngwele Muvengei, Lilian Wanjiku Manegene, Robert Akumu Asembo, na Saul Simiyu Wasilwa, ambao wataohojiwa siku ya Jumanne tarehe 25 mwezi huu.
Mwenyekiti wa jopo hilo Dkt Nelson Makanda amesema wale wanaotafuta nafasi ya makamishna watahojiwa kuanzia siku ya Jumatano tarehe 26 hadi Jumapili tarehe 30 na watu 105 wamejumuishwa katika orodha ya watakaohojiwa ili kujaza nafasa za Makamishna.
Dkt. Makanda amesema jopo hilo litafanya kila juhudi kuhakikisha wakenya wanapata makamishnaalio waadilifu na ambao wako tayari kufanya kazi bila ya kushurutishwa na mtu yeyote.
Dkt. Makanda amewarai wakenya ambao wako na dukuduku na watu walioorodheshwa kupigwa msasa kuwasilisha lalama zao kwa maandishi ili jopo hilo lichukue hatua za mapema.
“Wananchi wanaombwa kuwasilisha kwa maandishi na kiapo taarifa zozote zinazohusiana na wale walioorodhesha kuhojiwa kwa nafasi ya Mwenyekiti wa IEBC ili kuzuia kuteuliwa kwa viongozi wasio waadilifu”, Dkt Makanda.
National News
Chonga: Wakenya Wanaosafiri Ughaibuni Kusaka Ajira Hawazingatii Sheria za Leba

Mwenyekiti wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa Ken Chonga amesema baadhi ya wakenya ambao wanasafiri katika mataifa ya miliki za kiarabu kusaka ajira wamekosa kuzingatia sheria za Wizara ya Leba nchini na kuangukia mikononi mwa walaghai.
Chonga amesema ni lazima wakenya hao wachunguze mawakala wanaowasafirisha katika mataifa hayo kama wanatambulika na serikali, ndipo waingie katika mikataba ya uajiri ambayo imezingatia sheria za Leba nchini.
Akizungumza na Wanahabari mjini Kilifi, Chonga ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kusini amesema ili wakenya waepuke madhila mbalimbali kutoka kwa waajiri wao katika mataifa hayo ni lazima wasafirishwe na mawakala waliosajiliwa na serikali.
Wakati huo huo amesema japo serikali iko mbioni kuhakikisha inawatafutia wakenya kazi katika mataifa ya ughaibuni ni lazima wanaosaka ajira za ughaibuni waingie katika mkataba wa uajiri kabla ya kusafiri nje ya nchi.
National News
Chibule: Visa vya Dhulma za Kijinsi Vimepungua Kilifi

Serikali ya kaunti ya Kilifi imesema visa vya dhulma za kijinsia katika kaunti hiyo vimepungua kwa kiwango kikubwa.
Kulingana na Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Mbetsa Chibule, visa hivyo viliongezeka zaidi msimu wa maambukizi ya virusi vya Corona, ambapo kaunti ya Kilifi iliorodheswa nafasi ya tatu nchini baada ya kaunti ya Bungoma na Samburu.
Chibule amesema kwa sasa ni asilimia 12.3 pekee ya visa hivyo vilivyoripotiwa tofauti na asilimia 30 wakati wa maambukizi ya Corona, akisisitiza kwamba juhudi hizo zimefanikiwa kupitia ushirikiano wa jamii na wadau mbalimbali.
Kiongozi huyo amedokeza kwamba serikali ya kaunti imetoa mafunzo kwa maafisa wa kutoa ushauri nasaha ili kusaidia kupambana na visa hivyo mashinani, akisema juhudi hizo zitaendelezwa sawa na kudhibiti madhila hayo.
Wakati uo huo ameweka wazi kwamba kaunti hiyo imekamilisha ujenzi wa sehemu salama ya kuwahifadhi watoto wanaopitia dhulma za kijinsia wakati kesi zao zikiendelea Mahakamani.