Connect with us

National News

Mahakama Kuu Yamtupa Nje Gavana Mwangaza

Published

on

MAHAKAMANI – Gavana wa Meru Kawira Mwangaza amepata pigo baada ya Mahakama kuu kuidhinisha uamuzi wa bunge la Seneti la kumtimua Mamlakani.

Uamuzi huo imejiri baada ya bunge la Seneti kupiga kura kwa kauli moja na kuidhinisha malalamishi yaliowasilishwa na bunge la kaunti ya Meru dhidi ya kiongozi hiyo.

Malalamishi hayo dhidi ya Gavana Mwangaza ni pamoja na ukiukaji wa katiba, utumizi mbaya wa ofisi ya umma, ubadhirifu wa fedha miongoni mwa mashtaka mengine.

Akitoa uamuzi huo, Jaji wa Mahakama kuu Bahati Mwamuye, amesema Mahakama imeona kwamba ombi lililowasilishwa na Gavana Mwangaza la kupinga uamuzi wa bunge la Seneti halina uzito wowote na Mahakama ikatupilia mbali ombi hilo la Mwangaza.

“Mahakama hii imeona kwamba ombi lililowasilishwa na Gavana Mwangaza halina uhalali na kutulipiwa mbali. Notisi ya Gazeti la serikali iliyochapishwa tarehe 21 Agosti 2024 ya kumwondoa afisini imethibitishwa”, Jaji Mwamuye.

Mahakama imeamua kwamba bunge la Seneti halikukiuka maagizo yoyote ya Mahakama licha ya Gavana Mwangaza kulalamika kwamba bunge hilo liliegemea upande mmoja na kwamba Mahakama haikupata uthibitisho wowote juu ya madai hao.

Mahakama hata hivyo haikupata ushahidi wowote kwamba alinyimwa nafasi ya kuzungumza na ilibainisha kwamba timu yake ya mawakili haikuleta pingamizi lolote kuhusu muda uliotengwa kwa ajili ya utetezi wake.

Naibu Gavana wa kaunti hiyo ya Meru Isaac Mutuma M’Ethingia huenda akaapishwa rasmi na kuchukua nafasi ya Gavana katika kaunti hiyo ili kuhakikisha shughuli mbalimbali za kaunti zinaendelea vyema, iwapo Mwangaza hatakata rufaa kuhusu uamuzi huo wa Mahakama kuu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Chonga: Wakenya Wanaosafiri Ughaibuni Kusaka Ajira Hawazingatii Sheria za Leba

Published

on

By

Mwenyekiti wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa Ken Chonga amesema baadhi ya wakenya ambao wanasafiri katika mataifa ya miliki za kiarabu kusaka ajira wamekosa kuzingatia sheria za Wizara ya Leba nchini na kuangukia mikononi mwa walaghai.

Chonga amesema ni lazima wakenya hao wachunguze mawakala wanaowasafirisha katika mataifa hayo kama wanatambulika na serikali, ndipo waingie katika mikataba ya uajiri ambayo imezingatia sheria za Leba nchini.

Akizungumza na Wanahabari mjini Kilifi, Chonga ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kusini amesema ili wakenya waepuke madhila mbalimbali kutoka kwa waajiri wao katika mataifa hayo ni lazima wasafirishwe na mawakala waliosajiliwa na serikali.

Wakati huo huo amesema japo serikali iko mbioni kuhakikisha inawatafutia wakenya kazi katika mataifa ya ughaibuni ni lazima wanaosaka ajira za ughaibuni waingie katika mkataba wa uajiri kabla ya kusafiri nje ya nchi.

Continue Reading

National News

Chibule: Visa vya Dhulma za Kijinsi Vimepungua Kilifi

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imesema visa vya dhulma za kijinsia katika kaunti hiyo vimepungua kwa kiwango kikubwa.

Kulingana na Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Mbetsa Chibule, visa hivyo viliongezeka zaidi msimu wa maambukizi ya virusi vya Corona, ambapo kaunti ya Kilifi iliorodheswa nafasi ya tatu nchini baada ya kaunti ya Bungoma na Samburu.

Chibule amesema kwa sasa ni asilimia 12.3 pekee ya visa hivyo vilivyoripotiwa tofauti na asilimia 30 wakati wa maambukizi ya Corona, akisisitiza kwamba juhudi hizo zimefanikiwa kupitia ushirikiano wa jamii na wadau mbalimbali.

Kiongozi huyo amedokeza kwamba serikali ya kaunti imetoa mafunzo kwa maafisa wa kutoa ushauri nasaha ili kusaidia kupambana na visa hivyo mashinani, akisema juhudi hizo zitaendelezwa sawa na kudhibiti madhila hayo.

Wakati uo huo ameweka wazi kwamba kaunti hiyo imekamilisha ujenzi wa sehemu salama ya kuwahifadhi watoto wanaopitia dhulma za kijinsia wakati kesi zao zikiendelea Mahakamani.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.