News
Kesi ya Wakili Joseph Munyithia na Farid Salim Yachukua Mkondo Mpya

Kesi ya wizi wa ardhi inayomuhusisha Wakili Joseph Munyithia na mfanyabiashara Farid Salim Almaary imechukua mkondo mpya.
Hii ni baada ya mwanasheria huyo kuandikisha taarifa katika kituo cha polisi cha Makupa mjini Mombasa akijitenga na madai ya wizi wa kipande hicho cha ardhi kilichoko katika eneo la Shelly Beach eneo bunge la Likoni.
Katika taarifa yake kwa Polisi, Munyithia ameeleza kwamba alishughulikia ardhi hiyo ambayo alikabidhiwa hatimiliki na Gabriel Mutiso ambaye kwa sasa ni marehemu.
Aidha ameeleza kwamba mnamo Machi tarehe 4 mwaka 2024 alipeana cheti cha kukodisha shamba hilo pamoja na barua ya uhamisho hadi kwa kampuni ya J Katisya and Co Advocates.
Wakili huyo mkuu katika kampuni ya Munyithia, Mutugi na Umazi Advocates ameandikisha taarifa takriban wiki moja baada ya ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma nchini ODPP, kuagiza kukamatwa kwake pamoja na mfanyabiashara Farid.
Munyithia pamoja na mfanyabiashara huyo wanadaiwa kuiba na kuficha hati miliki ya ardhi hiyo kulingana na malalamishi yaliowasilishwa na wamiliki wa shamba hilo.
News
Mbogo: Kaunti ya Mombasa Imeshindwa Kutatua Mzozo wa Ardhi

Aliyekuwa mbunge wa Kisauni Ali Mbogo ameikosoa serikali ya kaunti ya Mombasa kwa kushindwa kutatua suala tata la uskwota linalowakumba wakaazi wengi wa kaunti hiyo.
Akizungumza katika eneo la Kisauni katika kaunti ya Mombasa, Mbogo amesema tatizo la uskwota limeendelea kuwa chanzo kikuu cha migogoro ya ardhi na ukosefu wa usalama katika maeneo mengi ya kaunti ya Mombasa huku serikali ya kaunti hiyo ikionekana kulifumbia macho suala hilo.
Mbogo amedai kwamba maelfu ya wakaazi wa Kisauni na Mombasa kwa jumla wanaishi kwa hofu ya kufurushwa katika ardhi zao walizoishi tangu jadi kufuatia ukosefu wa hati miliki.
Wakati huo huo amedokeza kwamba baadhi ya maafisa wa serikali ya kaunti hiyo wanahusishwa na visa vya uporaji wa ardhi za umma kwa kushirikiana na waekezaji jambo ambalo amelitaja kuwa dhulma.
News
Tuko Tayari Kufuzu Kombe La Dunia

Nahodha wa Kikosi cha Soka vijana chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 Rising Stars Amos Wanjala amesema kwamba lengo lao kuu ni kufuzu kombe la dunia kwenye fainali ya mashindano ya Afcon kwa chipukizi iliofungua milango yake weikndi hii mjini Cairo Misri.
Akizungumza akiwa kambini mjini Cairo Wanjala anamini kwamba wana kikosi bora cha kuandikisha matokeo chanya kwenye kombe hilo licha ya kuwa ni mara yao ya kwanza kushiriki katika kipute hicho.
“Tuko tayari kufuzu World cup maana tumekua tukijiandaa vyema kwa mashindano haya,nataka niwatoe hofu wakenya kwamba kundi letu ni la kifo kwani wawe tayari kupata burudani kutoka kwetu.”
kwa Mujibu wa tineja huyo wa academia ya Nasty Sports ya Uhispania ni kwamba licha mabadiliko ya hali ya anga akilinganisha na Kenya kila mmoja yuko tayari kuonyesha uwezo wake katika jukwaa hili.
“Tuko syched up kucheza na mpinzani yeyote,kila mmoja amejiandaa vizuri kutendea haki na kupeperusha bendera ya taifa letu. Nikitaka kushukuru wizara ya michezo pamoja na shirikisho kwa kutuunga mkono kuanzia mwanzo wa mazoezi yetu mpaka mandhari ambayo tumepata hapa.”
Vijana wa nyumbani wanafungua kampeni dhidi ya Morocco May 1 wakiwa kundi B pamoja na Tunisia na vilevile Nigeria