News
Kesi ya Wakili Joseph Munyithia na Farid Salim Yachukua Mkondo Mpya

Kesi ya wizi wa ardhi inayomuhusisha Wakili Joseph Munyithia na mfanyabiashara Farid Salim Almaary imechukua mkondo mpya.
Hii ni baada ya mwanasheria huyo kuandikisha taarifa katika kituo cha polisi cha Makupa mjini Mombasa akijitenga na madai ya wizi wa kipande hicho cha ardhi kilichoko katika eneo la Shelly Beach eneo bunge la Likoni.
Katika taarifa yake kwa Polisi, Munyithia ameeleza kwamba alishughulikia ardhi hiyo ambayo alikabidhiwa hatimiliki na Gabriel Mutiso ambaye kwa sasa ni marehemu.
Aidha ameeleza kwamba mnamo Machi tarehe 4 mwaka 2024 alipeana cheti cha kukodisha shamba hilo pamoja na barua ya uhamisho hadi kwa kampuni ya J Katisya and Co Advocates.
Wakili huyo mkuu katika kampuni ya Munyithia, Mutugi na Umazi Advocates ameandikisha taarifa takriban wiki moja baada ya ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma nchini ODPP, kuagiza kukamatwa kwake pamoja na mfanyabiashara Farid.
Munyithia pamoja na mfanyabiashara huyo wanadaiwa kuiba na kuficha hati miliki ya ardhi hiyo kulingana na malalamishi yaliowasilishwa na wamiliki wa shamba hilo.
News
Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.
Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.
Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.
News
Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.
Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.
Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.