Connect with us

National News

Washukuwa Wawili wa Kundi la Kigaidi la Alshabab Watiwa Nguvuni

Published

on

Watu wawili wanaoshukuwa kuwa wanamgambo wa kundi la kigaidi la Alshabab wametiwa nguvuni na maafisa wa kupambana na magaidi nchini ATPU katika kaunti ya Mandera.

Kulingana na maafisa hao, mshukiwa mmoja alifaulu kuvuka mpakani kutoka El-Adde nchini Somalia hadi nchini Kenya na kufanikiwa kupata kitambulisho cha kitaifa ili kutimiza malengo ya kigaidi.

Idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI imesema washukiwa hao wawili akiwemo Issac Mohammed Abdi na Noor Yakub Ali wote wakiwa na umri wa miaka 29, walikuwa wamepanga kuwateka nyara raia wa China waliokuwa wakitengeza mabomba ya maji katika uwanja wa ndege wa Mandera.

DCI imesema Mohammed alikuwa amepanga njama na mwandani wake humu nchini kumsaidia kumteka nyara raia wa China kwa gharama ya shilingi elfu laki moja ili kufanikisha mipango ya kusafirisha raia wa China hadi Somalia.

Maafisa hao wamesema baadaye walibaini kwamba gaidi mwengine Noor Yakub Ali, alikuwa amepanga kusaidia usafirisha wa utekaji nyara kwa gharama ya shilingi laki tatu hadi eneo la El-Adde nchini Somalia kabla ya njama hiyo kutibuka.

Washukiwa hao wanaendelea kuzuiliwa na maafisa wa kupambana na magaidi nchini ATPU kwa uchunguzi zaidi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Chonga: Wakenya Wanaosafiri Ughaibuni Kusaka Ajira Hawazingatii Sheria za Leba

Published

on

By

Mwenyekiti wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa Ken Chonga amesema baadhi ya wakenya ambao wanasafiri katika mataifa ya miliki za kiarabu kusaka ajira wamekosa kuzingatia sheria za Wizara ya Leba nchini na kuangukia mikononi mwa walaghai.

Chonga amesema ni lazima wakenya hao wachunguze mawakala wanaowasafirisha katika mataifa hayo kama wanatambulika na serikali, ndipo waingie katika mikataba ya uajiri ambayo imezingatia sheria za Leba nchini.

Akizungumza na Wanahabari mjini Kilifi, Chonga ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kusini amesema ili wakenya waepuke madhila mbalimbali kutoka kwa waajiri wao katika mataifa hayo ni lazima wasafirishwe na mawakala waliosajiliwa na serikali.

Wakati huo huo amesema japo serikali iko mbioni kuhakikisha inawatafutia wakenya kazi katika mataifa ya ughaibuni ni lazima wanaosaka ajira za ughaibuni waingie katika mkataba wa uajiri kabla ya kusafiri nje ya nchi.

Continue Reading

National News

Chibule: Visa vya Dhulma za Kijinsi Vimepungua Kilifi

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imesema visa vya dhulma za kijinsia katika kaunti hiyo vimepungua kwa kiwango kikubwa.

Kulingana na Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Mbetsa Chibule, visa hivyo viliongezeka zaidi msimu wa maambukizi ya virusi vya Corona, ambapo kaunti ya Kilifi iliorodheswa nafasi ya tatu nchini baada ya kaunti ya Bungoma na Samburu.

Chibule amesema kwa sasa ni asilimia 12.3 pekee ya visa hivyo vilivyoripotiwa tofauti na asilimia 30 wakati wa maambukizi ya Corona, akisisitiza kwamba juhudi hizo zimefanikiwa kupitia ushirikiano wa jamii na wadau mbalimbali.

Kiongozi huyo amedokeza kwamba serikali ya kaunti imetoa mafunzo kwa maafisa wa kutoa ushauri nasaha ili kusaidia kupambana na visa hivyo mashinani, akisema juhudi hizo zitaendelezwa sawa na kudhibiti madhila hayo.

Wakati uo huo ameweka wazi kwamba kaunti hiyo imekamilisha ujenzi wa sehemu salama ya kuwahifadhi watoto wanaopitia dhulma za kijinsia wakati kesi zao zikiendelea Mahakamani.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.