Connect with us

Entertainment

Young Njita: Mr. Malindi ni Brand Yangu ya Biashara – Wanaonilalamikia Wanahofia Mafanikio Yangu

Published

on

Msanii wa muziki wa rap kutoka Pwani, Ramadhan Ngao Mangale maarufu kama Young Njita – Njigiri, amezungumza kwa mara ya kwanza kwa kina kuhusu mgogoro unaomkabili kuhusu jina lake maarufu – Mr. Malindi.

Akiwa mgeni kwenye kipindi cha COCO ASUBUHI wakati akizindua EP yake mpya ya nyimbo 8 iliyopewa jina “1996” (mwaka wake wa kuzaliwa), Young Njita alisisitiza kuwa jina la Mr. Malindi si tu alilolichagua kwa mapenzi, bali limekuwa sehemu ya maisha yake ya kisanii, ya biashara, na ya jamii.

“Wanaonisema hawana hoja – wana wivu tu na mafanikio yangu. Jina hilo liliibuka baada ya kushinda tuzo ndani ya mji wa Malindi, na watu wenyewe wakaanza kunitambua hivyo. Nikaamua kulitumia kujenga brand yangu,” alisema kwa kujiamini.

Kwa mujibu wa Njita, jina hilo halihusiani tu na muziki. Limekuwa kivutio katika miradi mbalimbali ya kijamii na kibiashara kama vile: Ziara kwenye vituo vya watoto yatima (orphanages), Biashara ya boti, Uzalishaji wa filamu ya Mr. Malindi na Uuzaji wa nguo za chapa ya Mr. Malindi.

“Siwezi kuwa na jina ambalo lina nguvu kiasi hiki kisha niache tu kwa sababu watu wachache wamelalamika. Kila mtu anaweza kujiita Mr. Chonyi, Mr. Kilifi, hata Mr. Coast — hakuna anayemzuia. Jina la mji si milki ya mtu mmoja,” alisisitiza Njita.

Mgogoro huu ulizidi moto baada ya Lufdon Land, kampuni inayojihusisha na matukio ya urembo kama Miss Malindi, kuandika kwenye ukurasa wao wa Facebook tarehe 12 Mei:

“Tumeona jina la Mr. Malindi likitumika na msanii tajika toka Malindi. Jina hilo linamilikiwa kihalali na kampuni ya Lufdon Land… Tumekuwa tukimpa kazi msanii huyo, lakini hatukumchagua kama Mr. Malindi Kenya. Tunaomba kwa heshima asitishe kulitumia.”

Kampuni hiyo ilieleza kuwa hawafanyi shindano la Mr. Malindi kila mwaka, na linapofanywa, hupewa mshindi mmoja pekee. Kwao, jina hilo ni brand ya heshima na sura ya kampuni, hivyo kuliona likitumika kwenye biashara nyingine kuliwafanya wachukue hatua ya kutoa onyo hadharani.

Young Njita kwa upande wake anasema hali ya watu kumtaka aachane na jina hilo si kwa sababu ya sheria, bali kwa sababu ya mafanikio yake.

“Kila mtu anapigania jina baada ya kuona nimefanikiwa nalo. Mbona miaka yote walikaa kimya? Leo hii Mr. Malindi imekuwa gumzo kwa bidii zangu wanaanza kulalamika, kivipi?”

Hili ndilo swali kuu linalozua mjadala mkali mitandaoni. Je, jina kama Mr. Malindi linaweza kuwa milki ya mtu binafsi au kampuni moja? Au linapaswa kuwa huru kwa yeyote mwenye mapenzi, asili au mchango kwa mji huo?

Kwa sasa, bado hakuna tamko la kisheria lililotolewa wazi kuhusu uhalali wa usajili huo, lakini bila shaka, huu ni mgogoro unaoibua maswali mapya kuhusu haki za wasanii, biashara za majina, na nguvu ya brand binafsi zinazojengwa na watu wa kawaida.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Mboga Imejileta; Arrow Bwoy Aitisha Pigano Dhidi ya Shakib

Published

on

Msanii maarufu wa Kenya, Arrow Bwoy, amezua gumzo mtandaoni baada ya kumualika wazi wazi mfanyabiashara kutoka Uganda, Shakib Cham, kwenye pambano la ndondi.

Hii imekuja baada ya kipigo cha hadharani ambacho Shakib alipokea kutoka kwa msanii mwenzake wa Uganda, Rickman, hali iliyoacha mashabiki wengi wakisema: “Sasa ata Arrow Bwoy anaweza!”

Kupitia video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Arrow Bwoy, anayefahamika kwa vibao kama Digi Digi, hakuonyesha woga wowote. Kwa ucheshi, alisema amekuwa akisubiri nafasi kama hii kwa muda mrefu.

“Mboga imejileta,” alisema kwa kujiamini, akimaanisha kuwa Shakib amejileta mwenyewe kwenye kipigo.

“Chakula kiko tayari. Niko tayari kwa pambano hili.”

Arrow Bwoy pia hakusita kumtaja mke wa Shakib, Zari Hassan, akimtaka akae mbali na ulingo siku ya pambano hilo kwa usalama wake binafsi.

“Zari, usijisumbue kuja. Hii si sehemu ya wanawake. Usije ukazimia tukapata janga la pili,” alisema kwa kejeli.

Hata hivyo, wakosoaji wake walikumbusha jamii kuhusu video za awali zinazoonyesha Arrow Bwoy akichapwa na polisi wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha. Swali likabaki: Je, kweli ana uwezo wa kumpiga Shakib au ni porojo za mitandaoni?

Kwa jina la Zari kuingizwa kwenye sakata hili, mvutano umeongezeka na mashabiki kote Afrika Mashariki wanasubiri kuona kama Shakib atakubali changamoto hii ya kihistoria.

“Zari, kama unasikia, mtume tu kijana wako aje achukue kichapo — kichapo cha kimataifa,” Arrow Bwoy alimalizia kwa msisitizo.

Kwa sasa, macho yote yako kwa Shakib. Je, atakubali changamoto hii na kuweka historia mpya ya burudani Afrika Mashariki?

Continue Reading

Entertainment

#CHAN2024: Savara, Zuchu na Eddy Kenzo Kutumbuiza Fainali ya CHAN 2024 Nairobi

Published

on

Mashindano ya CHAN 2024 yakielekea ukingoni, mashabiki wanatarajiwa kupata burudani ya aina yake kutoka kwa baadhi ya nyota wakubwa wa muziki Afrika Mashariki.

Kenya, Uganda na Tanzania zitawakilishwa vilivyo kupitia majina makubwa matatu: Savara wa Kenya (mwanachama wa zamani wa kundi maarufu Sauti Sol), Eddy Kenzo wa Uganda, na Zuchu kutoka Tanzania, anayejulikana kwa jina halisi Zuhura Othman.

Onyesho hili la kufunga pazia litafanyika sambamba na mechi ya fainali Jumamosi, likitarajiwa kuhamasisha na kuburudisha maelfu ya mashabiki watakaofurika uwanja wa Kasarani. Shoo hiyo inalenga kumaliza mashindano haya ya kihistoria kwa upekee na kiwango cha juu cha burudani.

Mbali na kusubiriwa kwa hamu jukwaani, Savara pia amekuwa na mchango mkubwa nyuma ya pazia. Yeye ndiye mtunzi na mtayarishaji wa wimbo rasmi wa CHAN 2024 unaoitwa “Pamoja”.

Wimbo huo unashirikisha nyota kutoka kanda hii: Elijah Kitaka wa Uganda na Phina wa Tanzania. Uliimbwa kwa mara ya kwanza katika sherehe za ufunguzi na uliweka ladha na hamasa ya mashindano haya.

Ingawa wenyeji wa mashindano haya—Kenya, Uganda na Tanzania—waliishia katika hatua ya robo fainali, fainali za mwaka huu zinaahidi kuwa kilele cha msisimko.

Burudani kutoka kwa Zuchu, Savara na Eddy Kenzo itakuwa chachu ya kuhitimisha mashindano yaliyojaa matukio na hisia.

Kwa upande mwingine, kumekuwa na malumbano mitandaoni kati ya mashabiki wa Kenya na Tanzania, hususan baada ya timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, kudondoshwa nje ya michuano hiyo katika robo fainali.

Mashabiki wa Tanzania hawakusita kuchokoza wenzao kwa kejeli, jambo lililoongeza ladha ya ushindani wa nje ya uwanja.

Continue Reading

Trending