Sports
Waziri Wa Usalama Murkomen Asema Tuko Tayari Chan

Waziri wa Usalama wa ndaani Kipchumba Murkomen amesema kwamba Taifa la Kenya liko tayari kwa kipute cha CHAN mwezi ujao.
Akizungumza na wanahabari hapo jana Murkomen amesema miondo misingi ya usafiri na usalama iko tayari kwa sasa wakiwa tayari kulinda usalama wa timu zote na mashabiki nje na ndaani ya uwanja.
Murkomen pia amerai mashabiki kufika uwanjani kumiminika katika viwanja mbalimbali kupiga jeki kikosi cha Stars kuweza kufanya kweli kama mchezaji wa 12.
“Viwanja vya viko tayari hata zile za mazoezi kwa ajili ya Taji hili Spesheli,tuko tayari kulinda timu zote na wachezaji pamoja na mashabiki watakao kuja nchini kushabikia timu zao nchini,Pia Nichukue fursa kurai Wakenya kujitokeza kwa wingi kuwa mtu wa 12 kushabikia vijana wa nyumbani Harambee Stars.
Kwa mujibu wa Murkomen viwanja vyote vitakavyotumika vina usalama mkubwa na wanamikakati ya kuzuia tukio lolote ambalo linaweza tokea kwenye kipute hicho kwani wamejipanga vyema kabisaa.
Kombe hilo linangoa nanga Agosti 2 uwanjani Benjamin Mkapa nchini Tanzania.
Sports
Rais Ruto Awapa Morale Kikosi Cha Stars Kambini

Rais William Samoei Ruto mapema Leo ametembelea kikosi Cha timu ya Taifa Mpira wa Soka Harambee Stars Ugani Kasarani wanapofanyia mazoezi kwa Kombe la Chan 2025 mwezi ujao.
Hii ikiwa ni njia moja wapo ya kuwapa mortisha vijana wa nyumbani akiahidi Stars nchi nzima iko nyuma Yao.
Ruto amewatakia heri Stars na kuambia vijana wa nyumbani watapata sapoti yoyote wanayohitaji kutoka kwake wanapo peperusha bendera ya taifa hili kwenye kipute cha CHAN mwezi ujao.
“Nataka tushinde kombe hili katika nchi yetu,kila Mkenya yuko nyuma yenu kuwapiga jeki ili mpate matokeo chanya mimi na serikali yangu tunahidi kuwapa sapoti yote kwa kombe hili.”
Rais aliandamana na Waziri wa Michezo Salim Mvurya pamoja na waziri wa Ulinzi Soipan Tuya.
Vijana wa nyumbani wanafungua kampeini Agosti 3 dhidi ya DR. Congo ugani Kasarani ambapo watapiga mechi zao zote.
Sports
Kasarani Na Nyayo:Uwezo Wa Kubeba Mashabiki Yapungua

CHAN Siku 17 zimesalia kipute hicho kungoa nanga nchi za Kenya,Uganda na Tanzania.
Serikali ya Kenya kupitia Wizara ya Michezo imetumia Kima Cha zaidi ya Shilingi Bilioni 6.7 kufanyia Ukarabati uwanja wa Kasarani na Shilingi nyingine Bilioni 1.1 Uga wa Nyayo.