Connect with us

Business

Waziri Miano Asisitiza Ushirikiano Kati ya Serikali na Sekta Binafsi Katika Kuimarisha Utalii

Published

on

Waziri wa Utalii, Bi Rebecca Miano, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi katika kuandaa mpango wa pamoja wa kusaidia biashara na maeneo ya utalii nchini.

Akizungumza na wanahabari, Waziri Miano alisema kuwa sekta ya utalii nchini bado inakumbwa na changamoto mbalimbali, hivyo kuna haja ya kuweka mikakati madhubuti ili kuiimarisha na kuiwezesha kuchangia zaidi kwenye uchumi wa taifa.

Aidha, Waziri huyo alieleza kuwa kuna umuhimu wa kuwa na mfumo bora wa kudhibiti na kuboresha ubora wa huduma zinazotolewa katika sekta ya utalii. Alisema mfumo huo unapaswa kuzingatia pia mabadiliko ya tabianchi, ambayo kwa sasa yanaathiri pakubwa shughuli za utalii duniani.

Bi Miano alihitimisha kwa kusema kuwa kwa kuwepo kwa ushirikiano thabiti kati ya pande zote, sekta ya utalii inaweza kuwa chombo kikuu cha kukuza uchumi na kutoa ajira kwa maelfu ya Wakenya.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Published

on

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.

Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.

Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.

Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.

Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .

Continue Reading

Business

Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Published

on

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.

Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.

Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.

Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.

Continue Reading

Trending