Sports
Wanyonyi, Cherotich na Chepchirchir Washinda Fainali Diamond League Zurich, Kenya Yaandika Historia

Bingwa mtetezi wa Olimpiki katika mbio za mita 800, Emmanuel Wanyonyi, aliibuka mshindi wa taji la Diamond League baada ya kumshinda Max Burgin wa Uingereza katika fainali ya mbio hizo jijini Zurich, jana usiku.
Wanyonyi, ambaye anasubiri Kipute cha Dunia mjini Tokyo Japan ndani ya wiki mbili zijazo, alilazimika kutumia kasi ya mwisho ili kuzuia shambulizi la kasi la Mwingereza huyo katika hatua ya kumalizia. Akishinda kwa muda bora wa 1:42.37, huku Burgin akimaliza kwa muda wa 1:42.42.
Bingwa mtetezi wa Diamond League, Marco Arop wa Canada, alimaliza wa tatu kwa muda wa 1:42.57.
Ushindi wa Wanyonyi ukiashiria usiku wa kihistoria kwa Kenya, ambapo timu hiyo ilitwaa jumla ya medali tatu za Diamond League na medali ya fedha.
Mkenya mwingine Faith Cherotich, bingwa wa medali ya shaba Olimpiki, alidhibitisha umahiri wake kama malkia wa mbio za 3000m kuruka viunzi na maji, akitetea taji lake kwa muda wa 8:57.24.
Akiwa amefunzwa na Bernard Rono katika kituo cha mazoezi cha Kalyet, Kericho, bingwa wa zamani wa dunia kwa vijana aliwashinda kwa ufasaha Norah Jeruto mwenye asili ya Kenya lakini anayewakilisha Kazakhstan (9:10.87), na Marwa Bouzayani wa Tunisia (9:12.03).
Kocha Rono alimpongeza akisema: “Tulikuwa na malengo, na taji la Diamond League lilikuwa shabaha kuu. Sasa tuna siku chache kurekebisha maandalizi yetu kabla ya mashindano ya Dunia.”
Mwanariadha Nelly Chepchirchir, anayefundishwa na gwiji wa mita 800 Janeth Jepkosgei, aling’aa katika mbio za mita 1500 wanawake, akipiga kasi ya ajabu katika raundi ya mwisho na kutwaa taji lake la kwanza la Diamond League.
Alikimbia kwa muda wa 3:56.99, baada ya kumpita Jess Hull wa Australia, aliyekuwa anaongoza mbio kwa muda mrefu lakini akalemewa mwishoni.
Vijana pia walionesha makali, ambapo Edmund Serem mwenye umri wa miaka 17, mdogo wake Amos Serem (bingwa wa Diamond League 2024), alionesha kina cha vipaji vya Kenya katika mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji.
Serem mdogo alikimbia 8:09.96, akinyakua fedha, nyuma kidogo ya Frederik Ruppert wa Ujerumani (8:09.02). Tayari akiwa sehemu ya kikosi cha Kenya kitakachoshiriki mashindano ya Dunia mjini Tokyo, kijana huyo alionesha yuko tayari kuwakabili wakali wa dunia.
Sports
Shirika la Kupiga Vita Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) Lawashtaki Kenya kwa Kukosa Kutii Kanuni

Shirika la Kupambana na Matumizi ya Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) siku ya Alhamisi limeshtaki Kenya kwa kutotii masharti yake, hatua inayoweza kusababisha nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwekewa vikwazo mwezi ujao.
WADA, lenye makao yake Montreal, Canada, limesema kuwa shirika la kitaifa la kudhibiti matumizi ya dawa za kusisimua misuli nchini Kenya bado halijashughulikia mahitaji muhimu yaliyoainishwa baada ya ukaguzi uliofanywa mwezi Mei 2024.
Kwa sasa, Kenya ina siku 21 za kupinga madai hayo au kufanya marekebisho yanayohitajika na WADA, la sivyo itatangazwa rasmi kuwa imekosa kutii kanuni.
Kwa sasa, kuna wadau wanne waliotia saini kanuni za WADA walioko kwenye orodha ya kutotii masharti. Hawa ni pamoja na:
-
Urusi
-
Sri Lanka
-
Shirikisho la Kimataifa la Basque Pelota
-
Shirikisho la Kimataifa la Mazoezi ya Mwili na Ujenzi wa Misuli (IFBB)
Sports
Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya Ronald Bukusi Afafanua Hali ya Ukocha katika Timu ya Taifa

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya, Ronald Bukusi, ameondoa uvumi kuhusu mpangilio wa uongozi ndani ya timu ya taifa ya kriketi ya wanaume, akisisitiza kuwa hakuna mkanganyiko wowote kuhusu majukumu ya makocha Joseph Angara na Lameck Onyango.
Akizungumza katika makao makuu ya shirikisho hilo Ruaraka, Nairobi, Bukusi alieleza kuwa benchi la kiufundi linafanya kazi kwa mshikamano, huku wachezaji hao wa zamani wa kimataifa wakikamilishana katika uwezo wao.
“Tuna makocha wawili. Inategemea tu wanachofanya siku hiyo maalum,” alisema Bukusi.
Kwa sasa, Angara ndiye kocha mkuu, huku Onyango akiwa msaidizi wake. Wawili hao walichukua majukumu hayo kwa muda tangu Septemba 2024 baada ya bodi kufuta uteuzi wa mchezaji wa zamani wa India, Dodda Ganesh, kwa sababu za ukiukaji wa taratibu.
Kwa kuzingatia kuwa mashindano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la ICC la 2027 yanakaribia, Bukusi alisisitiza kuwa timu ya taifa imedhamiria kazi iliyo mbele yao. Mashindano hayo makubwa duniani yataandaliwa kwa pamoja na Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia.
“Kwa sasa, malengo yetu ni kujaribu kufika Zimbabwe na kufuzu Kombe la Dunia,” alisema Bukusi. “Tuna benchi bora la kiufundi linaloongozwa na Bw. Tariq [mwanabodi], na kwa pamoja tunashughulikia changamoto zinazoikumba timu.”
Hata hivyo, alionya kuwa mafanikio yanahitaji zaidi ya kipaji cha uwanjani, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utiifu wa kanuni katika mifumo yote.
“Lazima tuwe watiifu kuhusu fedha na kupiga vita matumizi ya dawa za kusisimua misuli. Sio kitu cha kufanikisha mara moja—itakuwa mchakato,” aliongeza.
Kenya itaendeleza kampeni ya kufuzu kwa kuikabili Namibia Septemba 26 katika Harare Sports Club, kisha kucheza dhidi ya Malawi Septemba 28 katika Takashinga Cricket Club. Mechi yao ya mwisho ya makundi itakuwa dhidi ya Nigeria Septemba 30.
Kenya inatarajia kurudia historia ya mwaka 2003, walipofika nusu fainali, mafanikio makubwa zaidi kuwahi kupatikana na taifa lisilocheza mechi za Test.
-
Entertainment6 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment18 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News15 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni