News
Wanasiasa wahimiza wakaazi kuunga mkono Serikali

Baadhi ya viongozi wa kisiasa katika kaunti ya Taita Taveta sasa wanashinikiza wakaazi wa kaunti hiyo kuunga mkono serikali ya Kenya Kwanza wakisema inaendeleza mikakati kuhakikisha inatekeleza miradi ya maendeleo katika kaunti hiyo.
Wakiongozwa na Mwakilishi wa wadi ya Chawia Joseph Mabishi alisema serikali ya Kenya Kwanza imeonyesha nia ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika kaunti hiyo na pwani kwa ujumla sawa na kutoa nafasi za kazi serikalini, hivyo kuna haja ya kuiunga mkono na kuipa muda ili ifanikishe ahadi zake kwa wananchi.
Aidha, Mabishi aliwataka viongozi wa kaunti hiyo ya Taita Taveta kuwa na agenda ya kuwahudumia wananchi badala ya kuwagawanya kupitia mirengo yao ya kisiasa.
‘’Tunataka viongozi ambao wanakuja kuleta nchi pamoja na kutujumuisha na pia kutekeleza maendeleo, sio wanasiasa wachochezi’’ Alisema Mabishi
Vilevile, Mabishi alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Taita Taveta kuashirikiana ili kuiboresha kimaendeleo.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.
Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.
Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.
Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.
Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.
Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.
Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.
Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.
Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.
Taarifa ya Joseph Jira