Connect with us

News

Wanaosajiliwa Kwenye Mpango wa Kazi “Majuu” Waonywa.

Published

on

Waziri wa Leba nchini Dakta Alfred Mutua amewaonya vijana waliopata nafasi za ajira ughaibuni dhidi ya kujihusisha na visa vya utovu wa nidhamu.

Akizungumza wakati wa zoezi la kusajili vijana kwenye mpango wa ajira za nje nchi maarufu Kazi “Majuu” katika kaunti ya Kwale, Waziri Mutua alitaja hatua hiyo kwamba huenda ikachangia kandarasi zao kufutiliwa mbali sawa na kukabiliwa kisheria.

Mutua alidokeza kwamba kuna baadhi ya vijana ambao tayari wamerejeshwa nchini kufuatia visa vya utovu wa nidhamu

“Unaskia unawashwa unataka kuandamana, unataka kuwa mwanaharakati, unataka kuchochea ingia ndege uje hapa wikendi moja uandamane kila mahali hiyo kitu ikutoke urejee kazini, kwa sababu ukienda kufanya huko maandamano unaharibia wakenya wengine, kuna watu waliandamana huko nchi tofauti tofauti, wakenya kumi na tano wengi wakasimamishwa, wakaregeshwa nyumbani, unaandamana kwa nchi nyengine wanauliza mbona mkenya anaandamana na mganda haandamani, mbona mtanzania haandamani”, alisema waziri Mutua.

Akizungumzia suala la utumizi wa dawa za kulevya, Waziri Mutua amewataka vijana hao kukomesha uraibu huo kwani  hakuna taifa linaloshabikia matumizi ya dawa za kulevya.

“Hapa utafanyia ukaguzi wa kiafya kama umekuwa ukivuta bangi, madawa ya kulevya utaanguka, hata ukikataa kupatikana hapa ukifika ng’ambo  utapatikana, kwa hivyo kama unataka kwenda ng’ambo achana na bangi bwana”,aliongeza waziri Mutua.

Zoezi hilo lililenga vijana 800 kaunti ya Kwale na 3,500 eneo la pwani kwa ujumla.

Taarifa ya Joseph Jira

 

 

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mudavadi: Mazungumzo yanaendelea kuhusu mzozo wa Kenya na Tanzania

Published

on

By

Mzozo kati ya Kenya na Tanzania umeanza kutokota kufuatia ilani iliyotolewa siku ya Jumanne Julia 29, na serikili ya Muungano wa Jumhuri ya Tanzania.

Serikali hiyo ya Tanzania kupitia Waziri wa Biashara na viwanda nchini humo Selemani Jefo ilitoa ilani ya kuwazuia wafanyibiashara wa kigeni kuendelea kufanya baadhi ya biashara katika taifa hilo.

Kutokana na hilo, Waziri wa masuala ya kigeni nchini Musalia Mudavadi alisema juhudi zimeanza za kuishawishi serikali ya Tanzania kuondoa vikwanzo hivyo na kwamba Rais William Ruto anafanya mazungumzo na mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhusu suala hilo.

“Rais William Ruto ambaye ni Mwenyekiti wa Jumaiya ya Afrika Mashariki anafanya mazungumzo na rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na mwafaka utapatikana kwani pia suala la diplomasia ni mwafaka na hii tatizo tutatua kama serikali kupitia mazungumzo ya kidiplomasia”, alisema Mudavadi.

Kwa upande wake Waziri wa biashara na viwanda nchini Lei Kinyanjua alionya kwamba huenda serikali ya Kenya ikachukua hatua sawa na hiyo dhidi ya Tanzania iwapo taifa hilo la Afrika Mashariki halitaangazia upya vikwanzo hivyo.

Mzozo huo wa kidiplomasia umejiri siku moja tu baada ya Waziri wa biashara na viwanda nchini Tanzania Selemani Jafo kutangaza kwamba serikali ya Tanzania imepiga marufuku wafanyibiashara wa kigeni dhidi ya kufanya biashara ndogo ndogo nchini humu ili kuruhusu watanzania kujiimarisha kiuchumi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Ethekon: Sheria haijafafanua taratibu za kuwarudisha nyumbani wabunge

Published

on

By

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeweka wazi kwamba hakuna sheria inayofafanua misingi na taratibu za kuwarudisha nyumbani wabunge ama maseneta waliokosa kuwajibikia majukumu yao ya kikazi.

IEBC, ilieleza kwamba suala hilo ni kinyume cha Katiba na ubaguzi ikilinganisha hatua hiyo na uamuzi uliyotolewa na Mahakama kuu kuhusu kesi iliyowasilishwa Mahakamani na Taasisi ya Katiba dhidi ya Ofisi ya Mwanasheria mkuu kwa kuambatana na sheria ya uchaguzi ya 2011.

Katika taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na kutiwa saini na Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon, IEBC ilisema kutokana na kwamba hakuna mfumo wa sheria wa kuwarudisha nyumbani wabunge ama maseneta waliokosa kuwajibikia majukumu yao ya kikazi, wakenya wanaweza kutumia kipengele cha 104 cha Katiba na kuwarudisha nyumbani Wawakilishi wadi. 

Aidha alisema wakati bunge la kitaifa likifanya marekebisho ya sheria kuruhusu kurudishwa nyumbani Wawakilishi wadi, hakuna mwafaka wowote uliafikiwa wa kuruhusu wabunge kurudishwa nyumbani iwapo wamekosa kuwajibika. 

Hata hivyo Tume hiyo imeahidi kuwajibika kikamilifu katika suala hilo huku ikisema tayari imeliandikia barua bunge la kitaifa kuibuka na sheria ya kuwarudisha nyumbani wabunge wasiowajibika.

Haya yamejiri kufuatia malalamishi yaliowasilishwa na baadhi ya wakenya wanaotaka baadhi ya wabunge na maseneta kurudishwa nyumbani wa hivi karibuni akiwa Mwakilishi wa Kike kaunti ya Nairobi Esther Passaris akituhumiwa kuvunja sheria na kukiukaji wa Katiba lakini uamuzi wa Tume ya IEBC ni afuani kwake.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending