Connect with us

News

Wanaharakati wamepinga mchakato wa mazungumzo ya kitaifa

Published

on

Mashirika ya kutetea haki za kibinadamu kaunti ya Mombasa yamepinga mchakato wa mazungumzo ya kitaifa yakisema matatizo yanayowakumba wakenya tayari yanajulikana.

Wanaharakati hao wakiongozwa na mkurugenzi mkuu wa shirika la Vocal Afrika, Hussein Khalid walidai serikali ya Kenya Kwanza imeshindwa kutekeleza matakwa ya vijana wa kizazi cha Gen z licha ya ahadi tele baada ya maandamano ya mwezi Juni mwaka 2024 ikiwemo fidia kwa walioafariki katika maandamano hayo, kukabiliana na ufisadi pamoja na maafisa waliohusika wakabiliwe kisheria.

Wanaharakati hao pia walidai mazungumzo hayo ni njama ya kufumbia jicho matukio ya ukiukaji wa haki za kibinadamu nchini.

“Raila Amolo Odinga tekeleza makubaliano na serikali kuu. Na ikiwa utafanya hivyo hakuna haja ya mazungumzo ama chochote kile’’, alisema Khalid.

Vilevile, Wanaharaki hao walisema ikiwa serikali kuu iko na ushahidi iwakamate waliohusika na iwafungulie mashtaka kwa mujibu wa sheria.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

IEBC inaendelea kutambua vituo vya kusajili wapiga kura

Published

on

By

Maafisa wa tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wamesema wanaendelea na zoezi la kutambua sehemu za kuweka vituo vya kusajili wapiga kura hasa maeneo ya mashinani.

Afisa msimamizi wa tume ya IEBC eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi, Mohammed Bahero Aboud alisema juhudi hizo ni kuhakikisha zoezi la usajili wapiga kura litakaloanza rasmi Septemba 29, mwaka huu linafaulu.

Akizungumza mjini Kilifi, Bahero alisema tume hiyo inatumia mbinu mpya ya kutambua vituo vya jadi vya usajili wapiga kura na kuweka vituo vipya kulingana na mapendekezo ya sheria.

Wakati huo huo alidokeza kwamba tume ya IEBC imekuwa ikihamashisha wakenya kutokubali kushawishiwa na wanasiasa na kujisajili katika maeneo yasiokuwa yao hasa msimu huu ambao zoezi hilo linakaribia kuanza.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Kaunti ya Mombasa kukumbatia matumizi ya mfumo wa miale ya jua

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Mombasa imesema imeanza kutekeleza mpango wa kutumia nishati mbadala katika vituo vyote vya huduma za kaunti, kwa kuanza na mabadiliko ya mfumo wa taa hadi kutumia umeme wa miale ya jua.

Kwa mujibu wa waziri wa kawi, rasilimali asili na ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kaunti ya Mombasa, Emily Achieng, hatua hii inalenga kupunguza gharama za matumizi ya umeme na kuhimiza matumizi ya nishati safi na rafiki kwa mazingira.

Mbali na hilo, waziri huyo alisema kaunti inaendelea kuweka vifaa maalum vya kupima ubora wa hewa katika maeneo mbalimbali ya mji na ndani ya taasisi za umma.

Lengo ni kupata ushahidi wa kisayansi kuhusu kiwango cha uchafuzi wa hewa, na kuchukuliwa kwa hatua za kisheria kwa wanaokiuka sheria.

Vifaa hivyo tayari vimewekwa katika hospitali ya rufaa ya Coast General na baadhi ya shule ikiwa ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa kaunti, kujenga ustahimilivu dhidi ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi.

Mikakati hiyo pia itasaidia kaunti katika kufanya maamuzi kuhusu maeneo yanayofaa kuwekwa biashara fulani, ili kulinda wananchi dhidi ya maradhi yanayosababishwa na uchafuzi wa hewa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading

Trending