Connect with us

News

Wanaharakati wamepinga mchakato wa mazungumzo ya kitaifa

Published

on

Mashirika ya kutetea haki za kibinadamu kaunti ya Mombasa yamepinga mchakato wa mazungumzo ya kitaifa yakisema matatizo yanayowakumba wakenya tayari yanajulikana.

Wanaharakati hao wakiongozwa na mkurugenzi mkuu wa shirika la Vocal Afrika, Hussein Khalid walidai serikali ya Kenya Kwanza imeshindwa kutekeleza matakwa ya vijana wa kizazi cha Gen z licha ya ahadi tele baada ya maandamano ya mwezi Juni mwaka 2024 ikiwemo fidia kwa walioafariki katika maandamano hayo, kukabiliana na ufisadi pamoja na maafisa waliohusika wakabiliwe kisheria.

Wanaharakati hao pia walidai mazungumzo hayo ni njama ya kufumbia jicho matukio ya ukiukaji wa haki za kibinadamu nchini.

“Raila Amolo Odinga tekeleza makubaliano na serikali kuu. Na ikiwa utafanya hivyo hakuna haja ya mazungumzo ama chochote kile’’, alisema Khalid.

Vilevile, Wanaharaki hao walisema ikiwa serikali kuu iko na ushahidi iwakamate waliohusika na iwafungulie mashtaka kwa mujibu wa sheria.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending