Business
Wakulima Rabai Wageukia Kilimo cha Viazi Vitamu Kufuatia Mvua Chache

Wakulima wanaoendeleza kilimo biashara kutoka rabai kaunti ya kilifi wamegeukia kilimo cha viazi vitamu.
Kulingana na wakulima hao msimu huu wa mvua chache viazi vitamu vinafanya vizuri ikilinganishwa na msimu wa masika.
Wakizungumza na cocofm wamesema kwa sasa kilimo cha viazi vitamu hakina hasara kwani kinachukua mda mfupi kuwa kukomaa na pia hakitumii maji mengi.
Aidha wamewashauri watu wengi kujihusisha na kilimo ili kujiinua kiuchumi.
“Kilimo cha viazi vitamu sai kinafanya vizuri kwani huwa havihitaji mvua nyingi na huu ni msimu wa mvua chache hivyo tunatarajia kufanya vizuri hata hivyo tunawaomba watu wengi kuingilia kilimo ili waweze kjiinua.”
Business
Bei ya vitunguu katika masoko ya humu nchini kuongezeka

Bei ya Vitunguu katika masoko ya humu nchini huenda ikaongezeka hata zaidi kufuatia uhaba wa bidhaa hiyo.
Kufuatia hatua hiyo wafanyibiashara wa vitunguu humu nchini wamelazimika kuagiza bidhaa hiyo kutoka taifa jirani la Tanzania kufuatia kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.
Wakizungumza na vyombo vya habari, Wafanyibiashara hao walisema kuna uhaba mkubwa wa vitunguu jambo ambalo limefanya bei kupanda.
Kulingana na wakulima wa zao hilo, hawakupanda vitunguu kutakana na gharama ya juu ya mbegu pamoja na changamoto za mabadiliko ya hali ya anga.
Aidha walisema kuwa gharama ya Kilimo cha vitunguu imekuwa juu ikilinganishwa na mapato ya chini na ukosefu wa bei nzuri sokoni.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
KEMFRI kuanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki

Taasisi ya utafiti wa bahari na uvuvi nchini, KEMFRI, imeanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki, ili kuongeza upatikanaji wao na kuinua sekta ya uvuvi nchini.
Akizungumza jijini Mombasa, kaimu mkurugenzi mkuu wa KEMFRI, Dkt. James Mwaluma, alisema kuwa mradi huo unatekelezwa katika eneo la Shimoni kaunti ya Kwale na unalenga kuzalisha samaki wa thamani kubwa kama vile kamba, matiko, na aina nyingine ambazo upatikanaji wake ni nadra.
Dkt. Mwaluma alisema kuwa mbegu zitakazozalishwa kupitia mradi huo zitasambazwa kwa vikundi vya vijana na wanawake wanaojihusisha na shughuli za ufugaji wa samaki, ili kuwawezesha kujitegemea kiuchumi.
Aidha, aliwahimiza vijana kote nchini wakumbatie fursa zilizopo kwenye uchumi wa baharini akisema ni njia mojawapo ya kujikwamua kimaisha na kupambana na ukosefu wa ajira.
Taarifa ya Pauline Mwango