Connect with us

News

Maadhimisho ya ugonjwa wa Selimundu duniani

Published

on

Huku ulimwengu ukiadhimisha siku ya ugonjwa wa Selimundu maarufu Sickle cell Aenemia, ukosefu wa hamasa za kutosha miongoni mwa jamii umetajwa kuchangia ongezeko la kusambaa kwa ugonjwa huo hasa maeneo ya Pwani.

Kulingana na Daktari wa watoto wenye ugonjwa wa Selimundu na pia ni mtafiti katika taasisi ya utafiti wa matibabu nchini KEMRI kaunti ya Kilifi Mejumaa Mohammed, amesema kwamba watoto wengi wanaadhirika na ugonjwa huo pasi nao kutambua kwamba wanaugua Selimundu.

Daktari Mejumaa alibainisha kwamba baadhi ya dalili za ugonjwa huo kwa watoto huonekana miezi minne hadi sita baada ya mtoto kuzaliwa.

“Ni jukumu la wazazi kuwa makini na afya ya watoto wao kwani magonjwa mbalimbali ya kuchipuka na kuathiri afya ya mtoto hasa Selimundu huonekana baada ya miezi mine hadi sita na kwamba ni hatari kwa afya ya mtoto kama hutabainika kwa haraka”, alisema Mejumaa.

Msimamizi wa wagonjwa wa magonjwa yasioambukizwa John Mosi, alisema Kilifi ni baadhi ya maeneo yaliothirika pakubwa na ugonjwa huo huku akisema kwamba wazazi walio na chembechembe za ugonjwa wa Selimundu wanapooana huenda wakapata mtoto aliyeadhirika na ugonjwa huo.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Waziri Joho na Mvurya waonya wanyakuzi wa ardhi.

Published

on

By

Waziri wa madini na uchumi wa bahari nchini Ali Hassan Joho alisema serikali haitaruhusu tena wakaazi kufurushwa katika ardhi wanayoishi.

Akizungumza katika maeneo ya Mzambarauni mjini Mtwapa eneo bunge la Kilifi Kusini kaunti ya Kilifi, Joho alionya kwamba mabwenyenye wenye hulka ya kufurusha wananchi kwenye ardhi za umma kamwe hawataruhusiwa.

Joho alisema wananchi hawafai kuhangaishwa kwenye ardhi zao huku akiwatahadharisha maafisa wa serikali dhidi ya kushirikiana na mabwenyenye kuhangaisha raia kwenye ardhi zao.

Hii ni baada ya kuibuka malalamishi ya mabwenyenye kutaka kuwafurusha wakaazi wa Utange Kaunti ya Mombasa.

Kwa upande wake Waziri wa michezo na Sanaa nchini Salim Mvurya alidokeza kuwa serikali inapanga kununua mashamba ambayo hayatumiki ili kuyakabidhi ya wananchi.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Marekani yarusha makombora Iran, Trump akionya Tehran

Published

on

By

Marekani imerusha mabomu kwenye maeneo ya Vinu vya Nyuklia vya Iran yanavyojumuisha Fordo na kuharibu kabisa maeneo hayo hatua ambayo huenda ikachangia vita zaidi ya kimataifa.

Rais wa Marekani Donald Trump alisema maeneo hayo yanayojumuisha Fordo, yalipigwa na makombora ya jeshi la Marekani huku Marekani ikijiunga na mashambulio ya Israel dhidi ya mpango wa Nyuklia wa Tehran.

Katika hatuba yake vya vyombo vya habari, Rais Trump alisema kwamba ni lazima Iran isitishe vita na kukumbatia amani iwapo wanataka vinu vyao vya Nyuklia kutorushiwa makombora.

Picha kwa hisani

“Tayari tumevuruga na kuharibu vinu vya Nyuklia vya Iran na bado tutaendelea kurusha makombora ya kasi zaidi na kuharibu vinu vyote vya Nyuklia vya Iran iwapo makao ya Tehran hayatasalimu amri”, alisema Rais Trump katika hotuba yake.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya nje wa Iran Seyed Abbas Araghchi alilaani vikali shambulizi la Marekani na kusema kwamba ni shambulizi la kuchukiza na kwamba Tehran ina njia zote za kutetea uhuru wake.

“Matukio ya asubuhi ya leo ni ya kuchukiza na yatakuwa na matokeo ya milele. Kila Mwanachama wa Umoja wa Mataifa ni lazima ashtushwe na tabia hii hatari sana, isiyo ya kisheria bali ni tabia ya kihalifu,” alisema Seyed.

Seyed aliongeza kwamba Marekani ilifanya ukiukaji mkubwa wa Katiba ya Umoja wa Mataifa kama Mwanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending