News
Wakaazi wa wakosoa kauli ya Rais Ruto dhidi ya viongozi wa kidini

Baadhi ya wakaazi kutoka kaunti ya Mombasa wamepinga matamshi ya Rais William Ruto kuwa viongozi wa kidini wamekuwa mstari wa mbele kuwachochea vijana dhidi ya serikali ya Kenya Kwanza.
Kulingana na wakaazi, vijana wa kizazi cha Gen-z wamechukua hatua ya kuandaa maandamano ya mara kwa mara, kukemea vitendo viovu kupitia mitandao ya kijamii kutokana na hali ngumu ya maisha na ukosefu wa uwajibikaji miongoni mwa viongozi wakuu serikalini na wala sio viongozi wa kidini wamewachochea.
Wakaazi hao wamemtaka Rais Ruto kukubali kukosolewa na viongozi wa kidini kwani viongozi hao wamekua wakitekeleza wajibu wao wa kuikosoa serikali kwa njia ya Amani.
“Kusema kweli ni kama Rais hataki kukosolewa kwa sababu hawa viongozi wanafanya kazi yao na wamekua wakifanya hivyo hata kwa serikali zilizopita na kama wewe mtu hutaki kukosolewa itakuwaje?” … aliuliza mmoja wa wakaazi.
Wakaazi hao aidha wameshikilia kuwa kando na viongozi wa kidini wao pia kama wananchi wana haki ya kuikosoa serikali kwani ni jukumu lao kikatiba huku wakiapa kutonyamazia madhila yanayotekelezwa na viongozi.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Christine: Wahudumu wa afya 1,340 wapokea mafunzo Taita Taveta

Serikali ya kaunti ya Taita Taveta kupitia Wizara ya Afya inaendelea kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya wa nyanjani ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao bila vikwazo.
Naibu Gavana wa kaunti ya Taita Taveta Christine Kilalo alisema kuwa kati ya wahudumu hao 1,340 asilimia 75 tayari wanaendelea na mafunzo katika ngazi tofauti.
Kilalo aliahidi kushirikiana na wahudumu hao licha ya changamoto zinazowakabili nyanjani.
“Wamekubali wakafundiashwa ili waweze kutoa elimu ya afya na waweze kusaidia jamii kwa mambo ya usafi na pia kusaidia katika kuwasilisha ujumbe za kiafya na pia wakipata wagonjwa waweze kuwatuma mahali wanaweza wakapata huduma za matibabu’’, alisema Kilalo.
Wakati uohuo alidokeza kuwa serikali ya kaunti hiyo kwa ushirikiano na serikali kuu wameweka mikakati ya kuhakikisha wahudumu hao wanalipwa fedha ambazo zitawasaidia kujikimu kimaisha pamoja na familia zao.
“Tulikubaliana kama taifa asilimi 50 ambayo ni elfu mbili mia tano inalipwa na serikali kuu na asilimia 50 ambayo ni elfu mbili mia tano inalipwa na serikali ya kaunti na kama serikali tunaemda kukamilisha malipo’’, aliongeza Kilalo.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Francisca atoa wito kwa vijana kuwania nyadhfa za kisiasa

Waziri wa masuala ya kijamii na ukuzaji wa talanta katika serikali ya kaunti ya Kwale, Francisca Kilonzo ametoa changamoto kwa vijana hasa wa Kike kwenye kaunti hiyo kujitokeza kwa wingi ili kuwania nyadhifa mbalimbali za kisiasa katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027.
Kilonzo aliwataka kuwania nyadhfa za uongozi wa kaunti ya Kwale sawia na bunge la kaunti hiyo ili kuhakikisha idadi ya wanawake waliochaguliwa inaongezeka.
Kilonzo na Mwakilishi mteule katika bunge la kaunti ya Kwale Judy Kengo walisema ikiwa vijana hao watazingatia hilo kutakuwa na ongezeko la Wanawake serikalini.
‘’Na ni Kwale pekee ambapo unaona viongozi ambao wamechaguliwa ni kidogo ukilinganisha na zile kaunti zingine za maeneo ya kati miongoni mwa zingine viongozi ambapo idadi iko juu’’, alisema Kengo
Naye Afisa wa mipango katika shirika hilo Rachel Akinyi na mmoja wa wanawake katika kaunti hiyo, Furaha Nyuki wameitaka jamii kuwaunga mkono wanawake kwenye uchaguzi huo mkuu ujao.
Taarifa ya Janet Mumbi