Connect with us

News

Wakaazi wa Malindi wanataka serikali kubuni mbinu za kuhifadhi miili ya Shakahola

Published

on

Wakaazi wa Malindi kaunti ya Kilifi walijitokeza na kuishinikiza serikali ya kitaifa kubuni mbinu mbadala za kuhifadhi miili ya watu iliyofukuliwa katika makaburi ya msitu wa Shakahola.

Wakaazi hao walisema kwa sasa wanalazimika kususia huduma za makafani ya hospitali kuu ya Malindi ambako miili hiyo inahifadhiwa hadi sasa.

Aidha walisema kwamba miili ya watu iliyofukuliwa Shakahola bado imelimbikizana kwenye makafani ya hospitali kuu ya Malindi bila ya hatua zozote madhubuti kuchukuliwa kuhusu miili hiyo.

“Tunashangaa jinsi serikali inavyoendesha shughuli zake hasa katika makafani ya hospitali kuu ya Malindi kwani ni zaidi ya miaka sasa bado kuna miili imesalia katika makafani hiyo

Wengi wa wakaazi wanasema kuwa inawagharimu kusaka huduma hizo kwenye hospitali za kibinafsi ambazo zinawatoza ada za juu mno.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Joho, awahimiza wakenya kujisajili katika “Boma Yangu”

Published

on

By

Waziri wa Madini na Uchumi wa raslimali za bahari Ali Hassan Joho, aliwahimiza wakenya kujisajili katika mpango wa “Boma Yangu” ili kunufaika na nyumba za bei nafuu zinazojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Waziri Joho alipongeza mradi huo wa serikali, akisema unalenga kuwaondoa wakenya kutoka kwenye makaazi duni na kuwapatia makaazi bora yenye hadhi na mazingira salama ya kuishi.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa baada ya swala ya Eid-ul-Adha, Joho aliwahimiza wakaazi wa eneo la Pwani kuchukua hatua za haraka kujisajili ili wasikose fursa hiyo muhimu ya kuboresha maisha yao.

“Kuna huu mradi unaitwa Affordable Housing, huu mradi mmeona umefanywa mahali kwingi sana na sai usajili wa ule mradi ambao utafanyika pale VOK eneo bunge la Nyali, nyumba 1,976 zitajengwa na mambo mengine, nawasihi kwa heshima kubwa sana waingie kwa Boma Yangu wajisajili”, alisema Joho.

Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohamed Nur aliwahimiza vijana kujitokeza kwa wingi kutuma maombi ya nafasi za ajira katika mpango wa kazi mtaani kwa vijana.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

KHRC: Wasichana elfu moja ni wajawazito, Lamu

Published

on

By

Takribani wasichana elfu moja kaunti ya Lamu wameripotiwa kupata mimba za utotoni kati ya mwaka wa 2024/25 huku visa vingi vikichangiwa na dhulma za kingono na ndoa za mapema.

Kulingana na Masharika ya kutetea haki za kibinadamu la MUHURI pamoja na lile la Kenya Human Rights Commission, KHRC serikali imeshindwa kuwakabili kisheria wahusika huku waathiriwa ambao ni wasichana wadogo wakiendelea kuhangaika.

Takwimu kutoka kwa kamati ya jinsia kaunti ya Lamu, iliwasilisha kwa kamati ya kitaifa inayoangazia masuala ya dhulma za jinsia kuwa kaunti hiyo ilinakili visa zaidi ya 700 vya mimba za utotoni mwaka wa 2024.

Takwimu hioz pia ziliweka wazi kwamba visa vingine zaidi ya 200 viliripotiwa kati ya mwezi Januari na Mei mwaka huu wa 2025.

Kulingana na ripoti kutoka kwa baraza la kitaifa la kudhibiti magonjwa NSDCC ilieonysha kwamba wasichana wanarika zaidi ya 600 nchini walipata mimba mwaka 2023.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending